Roman Abramovich mmiliki wa timu ya Chelsea kwa mara ya kwanza baada ya miaka mitatu ameweza kuishuhudia timu yake ya Chelsea ikicheza ndani ya dimba lake la Stamford Bridge walipomenyeana na klabu ya Manchester United kwenye mchezo ulioisha kwa sare ya moja moja.
Japo hakuwezekana kukamatwa na kamera za uwanjani lakini alikuwepo kuangalia mpira huo ndani ya uwanja mtu wake wa karibu alitoa taarifa hiyo, Roman Abramovich yupo jijini London tokea wiki iliyoisha akimpokea raisi wa Israel kwenye dimba la Samford Bridge.

Abramovich hakuuzulia mchezo wowote wa klabu yake tangia mchezo wa 2018, baada ya kupata matatizo ya visa, na pia ni mwaka huo huo alipatiwa uraia wa Israel na alikwenda kuhudhuria mchezo wa fainali ya ligi ya mabingwa kati Chelsea na Manchester City nchini Ureno kwenye dimba la Estadio do Dragao.
Abramovich aliinunua klabu Chelsea mwaka 2003 na kuisaidia kuwa klabu yenye nguvu jijini London na ulaya kwa ujumla, Roman Abramovich anakadiliwa kuwa na utajiri wa $14.1 billion kulingana na taarifa zilizochapishwa na jarida la Forbes mwaka 2021.
Mabingwa Meridianbet hawajawahi kukuacha mnyonge hasa katika kipindi hiki cha msimu wa sikukuu, kasino maridhawa ya Carnaval Jackpot inakupa thamani ya dau lako. Kuwa mmoja wa washindi leo hii.


