Kocha wa Barcelona, Ronald Koeman anasema kuwa hali ya hewa iko shwari kabisa kwenye kikosi chake na wakati wote wachezaji wake wamekuwa na mtazamo chanya.
Barca wapo nyuma kwa pointi sita dhidi ya vinara wa ligi Atletico Madrid, wakiwa tayari wamepoteza mechi 4 kati ta mechi zao 12 chini ya Koeman ambaye alichukua nafasi ya Quique Setien.
Barca walipokea kichapo kutoka kwa wapinzani wao Real Madrid na Atletico, pia walipata kichapo kilichowashangaza wengi kutoka kwa Getafe na Cadiz.
Hata hivyo, walionesha kuboreka katika mecchi yao dhidi ya Real Sociedad ambayo walipata ushindi wa 2-1. Koeman anasema kikosi chake kipo shwari na mipango zaidi ni kuendelea kupata ushindi.
Kutokana na hali halisi ya klabu kwa sasa, baadhi walikuwa wanaamini kuna walakini kwenye hatma ya meneja huyu, lakini yeye anawaondoa hofu waliyopo nyuma yake kuwa mambo yapo shwari.
“Wakati wote nimeona hali shwari, licha ya mechi tulizopoteza. Ni rahisi kuwa na hali ya furaha ukiwa umeshinda.”
Mpango wa Koeman, ambao amesisitiza zaidi ni kuendelea kufanya mabadiliko chanya katika kikosi na kuendeleza ushindi. Wanaelekea kuingia dimbani Jumamosi hii dhidi ya Valencia, hii ni fursa ya kuthibitisha namna anavyokipamba kikosi chake.
BURUDIKA NA WANYAMAPORI WAKIIMBA NA KUPIGA VYOMBO VYA MUZIKI!
Kupitia Kasino ya Mtandaoni ya Meridianbet, furahia mchezo wa Forest Rock. Hapa utaburudika na umahiri wa wanyapori wanaoimba na kutumia vifaa vya muziki wa rock. Burudika huku ukijiwekea nafasi ya kutengeneza pesa ndefu kupitia Meridianbet!!
Hopemwaikuka
Ni jambo jema
Adelta
Koeman anajitahidi kikosi kikae sawa
warda
Naamini Koeman atafanya vizuri sana badae
Rahma
Abali njema
Sarah
Jambo jema
Dorophina
Barca kwa sasa inamatumaini makubwa
Issa
Barca inakaa sawa
Lydia Emmanuel Magoti
Vizuri Barcelona Mambo yashakuwa mazuri sasa
Saupha mohamed
Safi
Janeflora malisa
Safi
Tatu
Good news