Roy Keane ameelezea kusikitishwa kwake na ukosefu wa ubora unaonekana katika kambi ya Manchester United kufuatia sare ya 0-0 ya Mashetani Wekundu dhidi ya Chelsea Jumapili alasiri.
Chelsea walionekana kuwa bora siku hiyo, na ingawa timu ya Ole Gunnar Solskjaer ilikuwa na wakati wake pia, hakuna ulinzi uliovunjwa pale Stamford Bridge.
Seti zote mbili za washambuliaji hawakufurahia kile walichokifanya, na Legendari wa Man United Keane alizungumzia mechi hiyo “lenye kuchosha” baada ya filimbi ya mwisho.
Akizungumza na Sky Sports News, Keane alisema: “Ulikuwa mchezo mbaya, nilikuwa nikikasirika zaidi kadri mchezo unavyoendelea. Hakuna kujituma kuingia kwenye boksi. Ukosefu halisi wa ubora kwa United. Michezo mikubwa ambayo haizalishi magoli, hiyo lazima ilete wasiwasi.
“Wanajaribu kushinda, lakini michezo hii nadhani mawazo yao ni kwamba tusipigwe. Nadhani United wanaangalia timu zilizo nyuma yao kuliko kujaribu kushinda mechi na kuifukuzia Man City.”
Kwa mujibu wa Keane, Unapokuwa kwenye moja ya timu kubwa jukumu la kushinda mechi ni jambo muhimu zaidi, sasa jambo la kwanza mameneja huzungumza katika mahojiano baada ya mechi ni kwamba wamefurahishwa na kupata hati safi, timu nilizocheza zilitaka kufunga mabao.
Ni Muda wa Kuvuna Mkwanja na Jungle Jim and the Lost Sphinx
Hauihitaji kufikira mara mbili ni mchezo gani utakupatia mkwanja ndani ya kasino za Meridianbet. Jiunge sasa ufurahie Jungle Jim and the Lost Sphinx.
Venerose
United wanatakiwa mazoezi ya kutosha
warda
Yaani United wameniboa sana
Neema juma
Wameboa kweli
Angelina
Wametukera sana mashabiki wa United
Rahma
Wamezingua
Adelta
Manchester united wamezingua sana
Sarah
United hawaeleweki
Issa
United walikoss umakin
Hopemwaikuka
Kweli