Zikiwa zimesalia takribani saa 36 tu kuelekea kwenye fainali ya kombe la Europa League, Kocha wa Manchester United, Ole Gunnar Solskjaer amemsema kushinda taji kunaipa timu imani lakini pia inaipa hamu ya kutaka makombe zaidi.
Ole atakuwa kibaruani kujaribu bahati yake ya kushinda taji akiwa kama kocha wa Manchester United jumatano hii dhidi ya Villarreal, akiwa na imani kubwa ya kuchukua kombe hilo.
Mwaka huu umekuwa mzuri kwa Solskajer baada ya kuisadia timu yake kumaliza katika nafasi nne za juu za EPL, huku akiendelea kusubiri kubeba taji na timu hii. Mara ya mwisho United kuchukua kombe ilikuwa ni mwaka 2017, na Ole anaamini jumatano hii watabeba ndoo!
“Kushinda taji kunaweza kukupa imani lakini pia kukudany utake mataji zaidi. Unaposhinda vitu, unakuwa unataka zaidi, unataka kupata ule moyo wa kunyanyua makobe zaidi,” alisema Solskjaer.
Kocha huyu alimalizia kwa kusema kuwa anawaamini wachezaji wake na watawashangaza wengi. Kulikuwa na tetesi nyingi za kocha huyu kuachwa baada ya kusuasua katikati ya ligi lakini inaonekana ana maisha marefu bado pale OT.
BONASI YA 50% KILA SIKU KATIKA KASINO ZA EVOPLAY HAPA MERIDIANBET.
Meridianbet na Evoplay Kasino wanakupa bonasi ya 50% ya kiasi utakachoweka katika akaunti yako leo. Unasubiri nini ni wakati wa kupiga pesa sasa na Mabingwa.
Sahihi kabisa
Dawa kabisa