Suala la hatma ya Paul Pogba limeingia katika sura mpya, likiendelea kugonga vichwa vya habari za michezo huku wadau wakiwa na mitazamo tofauti.
Sifahamu wewe una mtazamo gani ya hili, Ally McCoist wa Talksport anaamini kuna tatizo United na Pogba anapaswa kuondoka.
Pogba ameendelea kuwa na msimu mgumu chini ya Ole Gunnar, huku akionekana kuwa sio tegemezi sana chini ya meneja huyu ambaye amekuwa akitumia kama ziada kwenye mechi nyingi hivi karibuni.
Meneja wake wa timu ya taifa, Didier Deschamps aliweka wazi kuwa ni wazi kuwa Pogba hafurahii nafasi yake United wala mda wake wa kucheza kwa sasa.
Tangia mwezi Januari, United wamekuwa na Bruno Fernandez, ambaye anachukua nafasi kubwa ya Paul Pogba. Fernandez amekuwa akiendana vyema na Scott McTominay na Fred. Hivyo nafasi ya Pogba imekuwa ni ziada kutokana na uwepo wa Fernandez na sababu zingine ambazo Ole Gunnar yeye anaona ni za msingi.
Swali kubwa ni kuwa, ikiwa Pogba anashindwa kupata nafasi kwenye kikosi cha kwanza cha Manchester United kuna haja ya yeye kusalia klabuni hapo?
Sasa Ally McCoist anasema kuwa, ipo wazi kuwa kuna tatizo kati ya pande hizo mbili, klabu na Pogba. Na suluhisho pekee la mgogoro huu ni Paul Pogba Kuondoka tuu kwa sasa.
Wewe una mtazamo gani juu ya hili? Achia Comment yako hapa chini. 😊
Jaribu sasa hapa Meridianbet. Ukiacha ukweli kuwa itakupa burudani maridadi, bado inakuhakikishia ushindi mkubwa. Kazi kwako kukusanya ushindi!



Fatuma kasomo
Asante kwa taarifa meridianbet
magdalena
dah pogba akiondoka united kutakuwa na pengo kubwa sana maana sizani kama atatokea wa kushika nafasi yake akafit
Elika
Pogba nae kama anataka kwenda huko na aende tuu
Shakila mrope
Jamani aiondoke abaki tu Manchester pengo lake ataziba nani sasa
Fatina mfingi
Kambi popote pogba kikubwa mshiko tyu!!
Adelta
Pogba kikubwa maslai
Dorophina
Pogba haongee na huongozi kama mda wake wa kutumikia man u umeisha ili akatafute klabu nyingine ya kuitumikia
Nasra
Aangalie maslai tu
Khadija
Pogba achukue maamuz sahihi
Tatu
Pogba angeenda zake kutafuta upepo mwingine hapo kiwango chake cha uchezaji kitashuka
Carolyn
Pogba amekua na msimu mgumu Sana bora ahame tu Man U
Mwajumah
Pogba kama anataka aende uko aende tu
Angelina
Pogba nae anatuchanganya
Samira
Na aondoke tu tumemchoka hana maajabu
Lydia Emmanuel Magoti
Uwamuzi niwake aende au asiende kwasababu mtu usimlazimishe mtuu badae mtu ujaujutia kuto fanya vizuri kwenye krabu Pogba Kama unataka kusepa wewe sepa tuu
Saupha mohamed
Kambi popote
Sabrina
Asepe tu pogba kashaitumikia man vyakutosha
Janeflora malisa
Uwamuz ni wake
Rahma
Masilai ndo Kila kitu hangalie maslai
Povel
Uwamuzi ni wake kubaki old Trafford au kwenda popote anapo pataka