Uongozi wa Klabu ya Simba umesema kuwa haukuwa na mpango wa kuachana na Sven Vandenbroeck ambaye alikuwa Kocha Mkuu wa Simba na alibwaga manyanga Januari 7.
Sven alisepa ndani ya Simba mazima ikiwa ni siku moja baada ya Januari 6 kuipeleka timu hiyo hatua ya makundi ya Ligi ya Mabingwa Afrika.
Ushindi wa mabao 4-0 dhidi ya FC Platinum umewapa tiketi Simba kutinga hatua ya makundi ya Ligi ya Mabingwa Afrika.

Aliyekuwa Mtendaji Mkuu ndani ya Klabu ya Simba, Crestius Magori amesema kuwa Mtendaji Mkuu wa Simba,(Barbara Gonzalez) alipigiwa simu na watu kutoka sehemu aliyokuwa anakaa Sven na kuambiwa kuwa amebeba kila kitu mpaka viatu.
“Hatukuwa na mpango wa kuachana na Sven ila yeye mwenyewe aliamua kuondoka na CEO,(Barbara) alipigiwa simu na kuambiwa kuwa mbona kocha amebeba kila kitu kutoka kwa watu wa sehemu aliyokuwa anakaa.

“Ilikuwa ni asubuhi wakati huo timu ilikuwa inajiaandaa kwenda Zanzibar kwa ajili ya kushiriki Kombe la Mapinduzi.
“CEO alimpigia simu Sven ambapo alisema kuwa bado yupo hana mpango wa kuondoka ila timu imeanza safari mchana ndipo anamwambia CEO kwamba kuna matatizo ya kifamilia anahitaji kuondoka.
“Hata ambapo aliambiwa kwamba kama ishu ni familia basi ilete hapa Tanzania kuna shule akasema kwamba ana ofa kibao ikiwa ni pamoja na Morocco ambapo ni karibu na Ublelgiji, sasa hapo hatukuwa na namna ikabidi tumuache aondoke,” .
Sven kwa sasa yupo ndani ya Klabu ya FAR Rabat ya Morroco akiwa ni kocha mkuu na Simba inanolewa na Kocha Mkuu, Didier Gomes raia wa Ufaransa.

Anayejaribu hawezi kutoka kapa Meridianbet! Kasino ya mtandaoni ya Meridianbet inakuhakikishia ushindi mkubwa kila unapojaribu kuingia mchezoni. Washindi hushindana, ingia mchezoni!



Sania
FAR Rabat waliongeza mkwanja kwa Sven au kuna mengine
Lydia Emmanuel Magoti
Nimamuzi yake yeye
Adelta
Sven aliona aondoke tu kwa sababu kule kuna maslai zaidi
Hopemwaikuka
Ni yy tu
Dorophina
Sven naona alikuwa anatafuta maslai yalipo
Khadija
Kwani kambi kokote
Magdalena
Sven alikuwa bado anatarii anatafuta penye mkwanja wa maana na ndo kilichomfanya asepe Simba baada ya kupapata penye unafuu wa mkwanja
Rahmal
Mamuzi anayo mwenyewe
Sarah
Maisha popote
warda
Nitammic sana kishingo