Sven Atoa Sababu ya Kagere Kukaa Benchi

Kocha Mkuu wa Simba, Mbelgiji Sven Vandenbroeck amefunguka kwamba straika wake, Meddie Kagere anakaa benchi kutokana na yeye kupanga na kuchagua timu kutokana na aina ya timu ambayo anaenda kukutana nayo kwenye mechi zao.

Kocha huyo ameongeza kwamba pia amekuwa akiangalia zaidi mafanikio ya timu yake katika kushinda na wala siyo mtu mmoja huku kila mchezaji aliye hapo anaweza kukaa benchi kutokana na atakavyokuwa anawaona wapinzani wake.

Kagere ambaye alikuwa mfungaji bora wa timu hiyo kwa msimu uliopita, amekuwa akikosa nafasi ya kuanza katika kikosi cha kwanza cha timu hiyo ikiwemo katika mechi ya Ngao ya Jamii mbele ya Namungo FC ambapo Simba walishinda mabao 2-0.

Sven amesema kwamba hakuna tatizo la Kagere kukaa benchi ndani ya timu hiyo kutokana na hali hiyo inaweza kumkuta mchezaji yeyote ndani ya kikosi hicho kwa sababu ya kuangalia mafanikio zaidi ya kikosi hicho kuliko mtu binafsi.

“Kuhusiana na Kagere wala hakuna tatizo lolote lile la yeye kukaa benchi kwa sababu hilo linaweza kumtokea kila mchezaji aliye hapa.

“Nachagua timu kutokana na mfumo ulivyo na namna tunavyocheza, sijui kwa nini watu wanazungumzia kuhusiana na mtu mmoja.

“Naangalia mafanikio zaidi ya timu, kama tunashinda iwe timu na hata tukipoteza ni kwa ajili ya timu na hata tuchukue mataji ni timu, siyo mtu mmoja.

“Lakini vilevile anaweza kutumika kwenye mechi zetu zinazokuja mbele na wengine wakakaa tu nje,” alimaliza Mbelgiji huyo.


SHINDA NA HI LO

Sasa hii ni rahisi zaidi kupata USHINDI! Unatabiri karata ipi ipo chini au juu, kisha unakusanya mkwanja wako.

Cheza sasa

42 Komentara

    Sawa sven kocha wa mabingwa wa nchi na tumekuelew THis is SIMBA next level

    Jibu

    Sven yupo sahihi yeye anachoangalia ni mafanikio ya timu na siyo mtu

    Jibu

    maamuzi ya kocha ni mazuri sana kwa ajili ya manufaa ya timu ila tatzo linakuja pale watu wanapozusha maneno ya sintofahamu

    Jibu

    Kagere hana mahajabu tena na ndio maana kocha amekua hana hunakini nae mwisho wasiku utasikia tu kagere kauzwa

    Jibu

    Tumekuelewa kocha Steve@meridianbettz

    Jibu

    Ni vzr

    Jibu

    Kocha yuko sahihi kabisa

    Jibu

    Kocha yupo sahihi watu wasilete maneno maneno yeye anachoangalia nani anafanya vizuri msimu huu nani apumzishe yupo kwa ajili ya kikosi kizima

    Jibu

    Mnatuficha tu .Ila mbona za chini ya kapeti tunasikia kagere alimpiga kocha😂😂😂😂😂

    Jibu

    Mahamuzi ya koch yaeshimiwe juu yy anawatambua vyema vijana wake!!

    Jibu

    Safi sana

    Jibu

    Kagere hana jipya ndio mana kawekwa benchi hana maajabu simkubal wala nn#Meridianbettz

    Jibu

    Kagere ameanza taratibu mwisho wa siku atasema anataka kuama mchezaji anamaamuzi gani ya kuchagua mechi ipi anayotaka kuchezea

    Jibu

    Approach ya Kocha Sven ni nzuri lakini moja kwa moja inamuathiri Kagere kwa kiasi kikubwa sana hasa ukiangalia kwa misimu takribani miwili amekuwa mfungaji Bora lakini kwa upande mwingine nadhani Mwalimu anataka kumjenga zaidi kisaikolojia Kagere baada ya sekeseke lake la power Bank kwani wengi tunaona alishuka kwenye kufumunia Nyavu.

    Jibu

    Akae tu benchi siku hizi hana maajabu

    Jibu

    Itamsaidia kujipanga vzuri tena

    Jibu

    Kocha upo vizuri

    Jibu

    Oky kocha sven naamini mambo yatakua mazuri zaidi maana sisi wana simba tunachotaka ni ushindi

    Jibu

    Simba next level

    Jibu

    Alichokisema kocha kipo sahii kagere sio Kama apangwi kocha anakili yake awezi kuwachezesha viungo hote kipindi chakwanza ndomana kocha anamwanzisha Boko kagere mmaliziaji Sasa yeye kagere anataka kuchezeshwa ote kipindi kimoja Sasa kocha amegutuka Sasa ivi amebadiri utandawazi ndomana ana muanzisha moja moja ana malizia Sasa kagere ana ona Kama apangwi ana wekwa benchi Sana ndomana anapaniki

    Jibu

    Naangalia mafanikio zaidi ya timu, kama tunashinda iwe timu na hata tukipoteza ni kwa ajili ya timu na hata tuchukue mataji ni timu, siyo mtu mmoja.

    Jibu

    Sawa tu tunachoitaji kikosi kizuri

    Jibu

    Kila kocha hua anamfumo na mbinu zake kwaiyo anajua aina gani ya wachezaji akiwatumi watafanya vile anachokitaka.

    Jibu

    Yuko sahihi kabisah Steven

    Jibu

    Wapi Kagere Kagere

    Jibu

    Wachezaji wot wazur na uwez kuchezesh wote lazm wengne wakae benchi

    Jibu

    Kauli ya Sven inaongeza tetesi kwamba wawili hao walikunjana hivi karibuni,pengine anajaribu wachezaji wengine waliosajiriwa hivi karibuni#meridianbettz

    Jibu

    Lakini vilevile anaweza kutumika kwenye mechi zetu zinazokuja mbele na wengine wakakaa tu nje,”

    Jibu

    Umeeleweka kocha

    Jibu

    Kagere hana jambo umri umesogea

    Jibu

    Lakini vilevile anaweza kutumika kwenye mechi zetu zinazokuja mbele na wengine wakakaa tu nje,”

    Jibu

    Approach ya Kocha Sven ni nzuri lakini moja kwa moja inamuathiri Kagere kwa kiasi kikubwa sana hasa ukiangalia kwa misimu takribani miwili amekuwa mfungaji Bora lakini kwa upande mwingine nadhani Mwalimu anataka kumjenga zaidi kisaikolojia Kagere baada ya sekeseke lake la power Bank kwani wengi tunaona alishuka kwenye kufumunia Nyavu.

    Jibu

    Wamwache kocha afanye yake

    Jibu

    hayo ni maamuzi yake kocha ss mashabiki yetu macho#meridianbettz

    Jibu

    Bonge la makala

    Jibu

    Kazi na umri

    Jibu

    Tumetoka kwa bale sasa kwa kagere

    Jibu

    Sie Tunataka ushindi tu Mengine Atajua mwenyewe

    Jibu

    Tumuache kocha hafanye kazi yake

    Jibu

    Kocha yuko sahii.

    Jibu

    Yupo sahihi Kocha

    Jibu

Acha ujumbe

Meridianbet
Privacy Overview

This website uses cookies so that we can provide you with the best user experience possible. Cookie information is stored in your browser and performs functions such as recognising you when you return to our website and helping our team to understand which sections of the website you find most interesting and useful.