Hadi Sir. Alex Ferguson alinyoosha mikono juu na kukiri kwamba amewashindwa. Wakati Barcelona wanaibutua Man United katika fainali ya UEFA mwaka 2011 pale Wembley, shoka Iniesta na mpini wake Xavi walimsimamia kooni. ‘Big g’ zake zikawa chungu. United walipiga shuti moja tu lilolenga lango, walikuwa na umiliki wa mpira wa asilimia 33 tu. Walizidiwa kila kitu na Barca kasoro kadi na rafu tu.
Baada ya mchezo Fergie alisema “Sijawahi kucheza na timu ngumu kama hii. Timu iliyokamilika kila eneo kama hii, sijawahi kuiona. Sijawahi kukutana na viungo wanaoelewana kama hawa. Kuna muda nilidhani wachezaji wangu wataanguka kwa kizunguzungu kwa namna mpira ulivokuwa unazunguka. Yule Xavi na Iniesta walitushinda ujanja kabisa.” Kumbuka hapo Barca walikuwa wanaipiga United kwa mara pili mfululizo katika fainali ya UEFA.
Kwasababu tupo na Xavi leo, tumuache huyu ndugu yake. Tutamrudia Iniesta siku nyingine. Xavi yeye alifika Barcelona mapema sana, akiwa na miaka 11 tu alijiunga na ‘La Masia’. Kwasababu alitokea katika familia bora kifedha, hakuwahi kulazimishwa kwenda shule. Wazazi wake walimshauri aweke nguvu zaidi kucheza mpira kuliko kusoma, walimuona akifanikiwa zaidi ndani ya uwanja kuliko darasani. Wakampeleka La Masia akaanze maisha ya soka.
Alikulia hapo akizitazama sana mechi za kingereza. Yeye mwenyewe anadai kuwa analihusudu sana soka la Paul Scholes. Basi akakulia katika academy ya La Masia. Alipokuwa na miaka 19, AC Millan walitaka kumsajili. Wakamuahidi mshahara mrefu na nafasi katika timu ya kwanza. Kumbuka enzi hizo AC Millan wanatesa Ulaya. Xavi alikuwa tayari kupokea hiyo ofa, baba yake vilevile alikubali. Ila mama yake alimuambia akiondoka Barcelona atavunja ndoa na baba yake. Waachane. Basi Xavi kwa kuiheshimu ndoa ya baba akaamua kubaki Barca.
Ni mume wa Nuria Cunirella, msichana aliyemgombania na Carles Puyol mwaka 2012. Puyol aliachana na mpenzi wake ili awe na Nuria, ila Xavi alimzunguka na kumpata Nuria. Walipofunga ndoa 2013, wachezaji wengi wa Barca walihudhuria ila Puyol hakuwepo. Mpaka leo inadaiwa hawana mahusiano mazuri. Mapenzi bwana!
SHINDA NA HI LO
Sasa hii ni rahisi zaidi kupata USHINDI! Unatabiri karata ipi ipo chini au juu, kisha unakusanya mkwanja wako.


Povel
Thnks meridian ilikuwah combination nzur Sana dimba la Kati na nilikuwah kizaz cha dhahabu Kwan walifanikiwah kutwaaa makombe yote yaliyokuwah mbele yao thnks meridian kwa update
Ernest
Xavi na Iniesta ni balaa lingine kwenye ulimwengu wa soka nadhani historia yako itadumu kwa muda mrefu.
magdalena
hawa vijana ni moto wa kuotea mbali wanajua sana tena sana
Dorophina
Hayo jamaa wapo vizuri hawataki masihara kabisa
Adelta
Xavi na inista Ni vijana wenye uwezo mzuri kwa ulimwengu wa soka
@meridianbettz
Sauda
Vijana wanajua hadi wamepitiliza
Janeflora malisa
History yao nzr sana
felister
hawa jamaa si watu wa mchezo mchezo
Zeiyana
Ki ukweli xavi aliupenda sana mpira ndio maana kipindi hanapo kua uwanjani hanacheza mpira kutoka moyoni..!
Tatu
Xavi na Iniesta ni moto wa kuotea mbali hakika wamecheza mpira mzuri
Shani
Xavi na lniesta ni jeshi kubwa akuna wa kupiga hili!
Mwanahamisi
Historia yao nzuri
Latifa juma mohamed
Historia nzuri
Caroline
Yess ndivyo wachezaji wanatakiwa kuwa.
Mwajumah
Jamaa wapo vizur sana sio watu wa mchezo mchezo#Meridianbettz
Nasra
Vzuri sana kwa hao jamaa
Fatina mfigi
Watu wapo makini!!
Elika
Miamba miwili hiyo naikubali sanaaa
aisha
Hawa vijana wako vizuri
lombo
saf
Lydia Emmanuel Magoti
Hawa jamaa nawakubali kinoma Sana wanajua wapambanaji
Flomena
Baada ya mchezo Fergie alisema “Sijawahi kucheza na timu ngumu kama hii. Timu iliyokamilika kila eneo kama hii, sijawahi kuiona. Sijawahi kukutana na viungo wanaoelewana kama hawa. Kuna muda nilidhani wachezaji wangu wataanguka kwa kizunguzungu kwa namna mpira ulivokuwa unazunguka. Yule Xavi na Iniesta walitushinda ujanja kabisa.” Kumbuka hapo Barca walikuwa wanaipiga United kwa mara pili mfululizo katika fainali ya UEFA.
Saupha mohamed
Vijana wapo vizurii
Shafii
Wadau wa soka tukiwaona hawa jamaa tunakumbuka ile fainali ya club bingwa 2011 jinsi gani walimfanya sir Alex kutetemeka Kama kapigwa short.
farida ahmadi
Wanahistoria nzuri Sana
JULIANA WILBARD ALEX
Safi
Amiri Kayera
Walikua bola San kipindi chao
Sadick
Xavi na Iniesta walitengeneza Chemistry bora kuwahi kutokea duniani#meridianbettz
Hope mwaikuka
Hao watu ni nomaaa
Devotha
Good newz
Issa
Viungo ambao hawajawahi kutokea spain
Genia Sikaluzwe
History zuri sana
David Pere
Thnks meridian ilikuwah combination nzur Sana dimba la Kati na nilikuwah kizaz cha dhahabu Kwan walifanikiwah kutwaaa makombe yote yaliyokuwah mbele yao
Isaya massawe
Wajamaa wana hatari hawaaaa
Khadija
hawa vijana wanajua sana#meridianbettz
Sabrina
Xavi na Iniesta sio poa wanabalaa zito kwenye soka
Ester jackson
Asante kwa nakala
warda
Namwonaga Xavi na Iniesta hawana bahati kabisa
Furahav
Habari nzuri.
Samiah
Safi