US Open 2020: Thiem na Osaka Mabingwa

Hayawi hayawi, sasa yamekuwa. US Open 2020 imemalizika kwa namna ya kipekee, michezo ya fainali ilikuwa na burudani ya aina yake. Thiem na Osaka mabingwa wapya wa Mashindano haya.

Kwa upande wa wanaume, Thiem alikuwa akichuana na Zverev katika fainali ya Grand Slam mwaka huu. Mchezo ambao Zverev alikuwa na nafasi kubwa ya kuutwaa ubingwa mwaka huu, alianza vyema ila alishindwa kumalizia ‘mkia’ wahenga wanasema.

Thiem alipata ushindi akitokea nyuma kwa seti mbili na kuibuka kidedea kwa matokeo ya 2-6 4-6 6-4 6-3 7-6 (8-6) dhidi ya Zverev ambaye pia ni rafiki yake tangu utotoni.

Thiem baada ya kumaliza mchezo dhidi ya Zverev na kutawazwa Bingwa wa US Open

Hii ilikuwa ni fainali ya kwanza kwa Zverev katika hatua ya Grand Slam lakini ilikuwa ni fainali ya 3 kwa Thiem kwenye Mashindano ya US Open baada ya kulikosa kombe hili katika fainali mbili alizocheza.

“Natamani tungekuwa na washindi wawili leo, wote tulistahili ushindi huu.” Thiem alimwambia Zverev.

Mwanadada Naomi Osaka alikuwa na wakati maridhawa alipokutana na gwiji Azarenka katika Fainali ya US Open 2020.

Osaka ameendelea kuonesha kiwango chake kinachozidi kukua siku baada ya siku. Hili ni taji lake la 3 la Grand Slam, 2018 alibeba kombe la US Open na 2019 akachukua Australian Open.

Naomi Osaka baada ya mchezo dhidi ya Azarenka

Osaka alishinda kwa jumla ya seti 1-6 6-3 6-3 na kubeba taji lake la 2 la US Open. Baada ya mchezo huu, Osaka alimtania Azarenka kwa kusema, ” Sitaki kucheza na wewe tena kwenye fainali nyingine yeyote,sijaufurahia mchezo, ulikuwa mgumu sana kwangu.

“Hili limekuwa tukio la kunivutia kwani nimekuwa nikikuona tu ukicheza kwenye kiwanja hiki wakati nikiwa mdogo, nimejifunza vingi, asante sana.”


SHINDA NA MERIDIANBET!

Tengeneza pesa kidijitali kwa kubashiri mbio za farasi hapa Meridianbet! Chagua nani ashinde, unakusanya mkwanja.

Cheza Sasa.

19 Komentara

    Huyu Naomi hatari kabisa ubigwa yeye utaji namba moja yeye jamani kunawata wananeema sana hongeza zake

    Jibu

    Ushindi ni haki yao.hivyo wanastahili pongezi kwa kazi nzur

    Jibu

    Osaka ameendelea kuonesha kiwango chake kinachozidi kukua siku baada ya siku. Hili ni taji lake la 3 la Grand Slam, 2018 alibeba kombe la US Open na 2019 akachukua Australian Open, so nice congr NAOMI OSAKA!!

    Jibu

    Osaka amefurahia sana huu Ushindi#Meridianbettz

    Jibu

    Zverev na azarenka wasivunjike moyo sana kwani hadi kufikia fainali juudi kubwa wamefanya kikubwa wajopange tu michezo bado hipo na hinaendelea

    Jibu

    Pongez kwao

    Jibu

    Hongera Sana Thiem na Osaka

    Jibu

    Haki yaho kupata ushindi wanapambana sana

    Jibu

    wamestahili ushindi ongera zao

    Jibu

    safiii

    Jibu

    Pongezi kwao,kazi nzuri wamefanya!!!

    Jibu

    Kazi nzuri aliyoifanya Naomi apewe pongezi kwa sasa naona hana mpizani

    Jibu

    Pongezi ziende kwao

    Jibu

    Wooh hongera zao

    Jibu

    Walk vzuri hongera kwao

    Jibu

    Osaka amefurahi sana

    Jibu

    pongezi nyingi sna kwao juhudi zao ndo zimewafikisha apo walipo

    Jibu

    SAfi

    Jibu

    Huyu Naomi hatari kabisa ubigwa yeye utaji namba moja yeye jamani kunawata wananeema sana hongeza zake

    Jibu

Acha ujumbe

Meridianbet
Privacy Overview

This website uses cookies so that we can provide you with the best user experience possible. Cookie information is stored in your browser and performs functions such as recognising you when you return to our website and helping our team to understand which sections of the website you find most interesting and useful.