Tetesi zinasema Mkufunzi wa Barcelona Ronald Koeman bado ana matumaini kwamba Lionel Messi atasalia katika klabu hiyo na kukataa kuingizwa katika mjadala kuhusu hatma ya baadae ya nyota huyo wa Argentina mwenye umri wa miaka 33.
Tottenham huenda ikawasajili wachezaji zaidi mwezi Januari na inatarajiwa kumtafuta mlinzi mpya wa safu ya kati, huku mchezaji wa kimataifa wa Colombia Davinson Sanchez, 24, akitarajiwa kuondoka.
Kiungo wa kati wa Mbrazil Willian, 32, ‘amechukuliwa hatua’ na Arsenal baada ya kwenda Dubai wiki kadhaa zilizopita – huku Mikel Arteta akisisitiza suala hilo ‘limesuluhishwa’.

Tetesi zinasema Jurgen Klopp anasisitiza kuwa hana habari kuwa mabingwa wa Ligi ya Premia Liverpool, wanapania kumnunua mlinzi mpya mwezi Januari dirisha la uhamisho litakapofunguliwa.
Liverpool wamefahamishwa kuwa watalazimika kulipa £26.7m ikiwa wanamtaka mlinzi wa Ajax Perr Schuurs, 20, huku AC Milan pia wakionesha nia ya kutaka kumnunua mholanzi huyo anayecheza safu ya kati na nyuma.
Mkufunzi wa Everton Carlo Ancelotti amepuuzilia mbali tetesi zinazoashiria anawataka wachezaji wake wawili wa zamani; kiungo wa kati wa Real Madrid na Uhispania Isco, 28, na kiungo wa kati wa Juventus na Ujerumani Sami Khedira, 33.
Tetesi zinasema West Ham pia wamehusishwa na mshindi wa zamani wa Kombe la Dunia Khedira.

Tetesi zinasema Kiungo wa kati wa Uswizi Granit Xhaka, 28, hana mpango wa kuondoka Arsenal kuelekea Inter Milan mwezi Januari.
Baba yake Erling Haaland, Alf-Inge, kiungo wa kati wa Nottingham Forest, Leeds na Manchester City, amekiri kuwa mwanawe ambaye ni mshambuliaji wa kimataifa wa Norway, 20, anatamani kujiunga Ligi ya Premier lakini kwanza anataka kushinda taji na klabu yake ya sasa, Borussia Dortmund.
Kiungio wa kati wa zamani wa Manchester City Trevor Sinclair, anaamini kuwasili kwa mchezaji nyota wa Barcelona Lionel Messi, 33, ‘hakutaepukika’ baada ya mkataba wa mkufunzi wa City Pep Guardiola kurefushwa.
Hauhitaji kuwaza linapokuja suala la ubashiri na odds kubwa. Bashiri na Meridianbet ukiwa popote ufurahie ushindi mkubwa katika michezo mbalimbali na hadi milioni 16 kwenye michezo ya kasino.



magdalena
barcelona wamuache messi ndo awe muamuzi wa maisha yake ya soka
Adelta
Messi ndiyo Kila kitu Barcelona
Lydia Emmanuel Magoti
Yani Barcelona bado Wana umizwa vichwa na Messi ivi Messi akitoka apo Barcelona kutakuwaje Barcelona ataweza kuendeshwa au ndompaka Messi awepo mwacheni tuu nayeye akangalie soka kwingine
Caroline
Messi roho yake haitaki kubaki Barca
Fatina mfingi
Messi kam kashachoka barcelona wamuache tyu afanye maamuz yake!
Povel
Nice update
Angelina
Goodupdate
Sauda
Makala bomba!!!
zeiyana
Dilisha la usajiri likifunguliwa sizani kama man u watakaa nyuma tena
Hopemwaikuka
Haya kaz kwao
aisha
Messi kwa gunzo
Latifa juma mohamed
Thanks for new updates.
Saupha mohamed
Good news
felister
habari njema
Sania
Good news
Tatu
Mess yupo vizuri
[email protected]
Mess ndio kila kitu Barcelona