Tetesi zinasema Arsenal wanamtaka mshambuliaji wa Real Madrid Isco, 28, katika dirisha la uhamisho la mwezi Januari litakapofunguliwa.
Kiungo wa kati wa Uholanzi Georginio Wijnaldum, 30, ataamua wiki hii iwapo atatia saini kandarasi mpya na klabu ya Liverpool huku kocha wa Barcelona Ronald Koeman akiwa na matumaini ya kumshawishi kiungo huyo kujiunga na Barcelona.
Manchester City boda ina matumaini itamsajili mshambuliaji wa Barcelona Lionel Messi 33, mwaka 2021, licha ya nahodha huyo wa Barca kusema kwamba anatumai kwamba siku moja atacheza soka nchini Marekani.
Mauricio Pochettino anatarajiwa kuwasajili baadhi ya wachezaji wa Tottenham ikiwemo kiungo mshambuliaji Dele Alli, 24, na kipa wa Ufaransa Hugo Lloris, iwapo kocha huyo raia wa Argentina atathibitishwa kuwa mkufunzi Paris-St Germain.
Wolves huenda ikawasilisha ombi la kumsajili Diego Costa, 32, kuchukua mahala pake mshambuliaji wa Mexico Raul Jimenez, 29, baada ya mshambuliaji huyo wa Uhispania kukubali kusitisha kandarasi yake katika klabu ya Atletico Madrid na kuwa mchezaji huru mwezi Januari.
Tetesi zinasema Tottenham inataka ya kumsajili kiungo wa kati wa Austria Marcel Sabitzer, 26, mwezi Januari kulingana na klabu yake RB Leipzig.
Tetesi zinasema Arsenal imesitisha mpango wa kumnunua mchezaji wa Lyon na Ufaransa Houssem Aouar wakati dirisha la uhamisho la mwezi Januari litakapofunguliwa.
Tetesi zinasema Liverpool imesitisha mpango wa kumsajili beki wa kati wa Inter Milan Milan Skriniar, 25, baada ya kukasirishwa na dau la £54m lililowasilishwa na klabu hiyo ya Italia.
Beki wa Chelsea na Uhispania Marcos Alonso, 30, anatarajiwa kurudi Uhipania na kujiunga na Atletico Madrid kwa mkopo katika dirisha la uhamisho la mwezi Januari . Alonso hajaichezea Chelsea tangu tarehe 26 Septemba.
Mkufunzi wa zamani wa England na Juventus Fabio Capello anasema kwamba atabadilishana mshambuliaji wa Argentina Paulo Dybala, 27,na mshambuliaji wa Tottenham na England Harry Kane, 27.
VUNA SHEA YAKO YA 230,000,000TSH NA UFURAHIE MSIMU HUU WA SIKUKUU!!!
Kupitia Kasino ya Mtandaoni ya Meridianbet, jiwekee nafasi ya kupata shea yako ya 230,000,000Tsh kupitia mchezo wa Secret Santa. Hakika hutojutia kufurahia msimu huu wa sikukuu ukiwa katika nyumba ya mabingwa ya Meridiabet. Unasubiri nini?
warda
Wajitahidi watampata
Tatu
Sijui kama mess atakubali kwenda man city
Fatina mfingi
Mmmh sio kweli messi kutoka hapo alipo
Chiku
Mess akomae
Mwanahamisi
Mess bora awadindie asichomoke kwenda kokote
Sarah
Mess hawezi kutoka hapo
Angelina
Goodupdate
Rahmal
Mmmhhh mess kutoka awezi ila sijui
Hopemwaikuka
Juve fanyen huo mpango
Caroline
Asante kwa taarifa
Angelina
Goodupdate
Dorophina
Nice update
David Pere
Ni hekaheka tu za usajili
Zahara omary
Imekaa poa snaa
Lydia Emmanuel Magoti
Zipo poa
Sania
Messi atulie na timu yake
Sabrina
Messi hapo kashafika