Tetesi za Usajili

Kocha wa Aston Villa, Dean Smith anakusudia kukiimarisha kikosi chake katika safu ya ushambuliaji baada ya kufanikiwa kuepuka kushuka dara kutoka Premier League.

Katika kuhakikisha inafanikiwa katika hilo, wamekusudia kumsajili mshambuliaji wa Liverpool, raia wa Ubelgiji Divock Origi, 25.

Origi amefanikiwa kucheza jumla ya michezo 44 pekee ndani ya Liverpool msimu huu uliyomalizika, lakini mara zote amekuwa mtu wa kusugua benchi akiwapisha Mo Salah, Sadio Mane na Roberto Firmino wakianza.(Sun)

Mabingwa wa kombe la FA klabu ya Arsenal wanamlia rada beki wa kati raia wa Brazil, Diego Carlos huku Mikel Arteta akikusudia kukisuka upya kikosi chake kwaajili ya msimu ujao. (Telegraph)


Arsenal inatarajia kutoa ofa nono kwa mshambuliaji wake raia wa Gabon, Pierre-Emerick Aubameyang 31, wiki hii ya pauni milioni 250,000 kwa wiki katika makubaliano ya miaka mitatu kuendelea kusalia kwenye klabu hiyo. (Mirror)

Kocha wa Tottenham Jose Mourinho amepewa fursa ya kumsajili mshambuliaji wa Watford Troy Deeney, 32, kuchukua nafasi ya Harry Kane kwa muda. (Mail)

Liverpool imeitangulia Paris St-Germain katika kinyang’anyiro cha kutaka kumsajili Thiago Alcantara wa Bayern Munich na sasa hivi ina uwezekano mkubwa wa kumsajili kiungo wa kati wa Uhispania. (Mundo Deportivo, via talkSPORT)

Mtendaji Mkuu wa Manchester United Ed Woodward amefanya mazungumzo na wawakilishi wa mchezaji wa Lille Gabriel Magalhaes juu ya uhamisho wa mlinzi huyo wa Vrazil, 22. (RMC Sport, via Express)

Wakati huohuo, United inamatumaini ya kumtumia mlinzi Chris Smalling, 30, katika makubaliano ya mabadilishano na mlinzi wa Inter Milan, 25, raia wa Slovakia Milan Skriniar – lakini Roma inaendelea na machakato wake wa kumtafuta Mwingereza baada ya kuiridhisha timu hiyo alipokuwa kwa mkopo. (Star)


Tiketi yako ya kwanza kamwe haiwezi kupoteza ukiwa na Meridianbet. Unarudishiwa 100% ya Tiketi yako ya kwanza.

Ingia mchezoni

30 Komentara

    Habar njema sana 👍

    Jibu

    Aston villa amchukue tu origi.

    Jibu

    Habar nzur

    Jibu

    Tetesi zimekaa poa.

    Jibu

    Safi sana

    Jibu

    Bonge la makala

    Jibu

    Asante Sana meridianbet

    Jibu

    Habari nzuri

    Jibu

    Habari nzuri #meridianbettz

    Jibu

    aston villa pamoja na kufanya usajili wanatakiwa waongeze juhudi katika kufikia viwango bora kimpira

    Jibu

    Aston villa msimu ujao inabidi waimarisha kikosi kiwe poa zaidi wasije wakashuka daraja

    Jibu

    Habari njema hizi kwawale wa mchezaji ambao wako benchi kusajiliwa kwao inawapa fursa ya kwenda kuonyesha kuwa nao walikuwa bora kuwepo uwanjani pale walipo kosa nafasi hizo

    Jibu

    Hongera sana kocha wa Aston villa kwa kuimalisha kikosi chako ni jambo la maana sana ambalo umeliamua

    Jibu

    Hapo watakuwa wamefanya vizuri #Meridianbettz

    Jibu

    Jinsi gani arsenal walivyo samini huwepo wake aubameyang

    Jibu

    Aston villa inabidi wasijili msimu ujao ili kuimarisha kikosi zaidi

    Jibu

    Hii ya aston villa hii na mashaka na forwald wetu mbwana samatta kukosa namba au kutolewa kwa mkopo baada ya kuonyesha kiwango kibovu pale villa park akija orig kutoka liverpool

    Jibu

    Habari njema

    Jibu

    Hakika hi ni Habali njema

    Jibu

    Thiago Alcantara amekuwa Lulu mara Man City,mara Liverpool na sasa nasikia PSG#meridianbettz

    Jibu

    Habari njema#meridianbettz

    Jibu

    Aston villa kumchukua orig sidhan kama samata atakuwa na nafasi hapo

    Jibu

    Hawa Arsenal hawa kama yangaa

    Jibu

    Habar njema

    Jibu

    Good

    Jibu

    Good news

    Jibu

    Imeeleweka hii

    Jibu

    Binafsi naliangalia hili deal la Divock Origi kama ni ishara nzuri kwa Origi kwani atapata muda mwingi wa kucheza tofauti na anavyopewa Liverpool

    Jibu

    Habari njema sana

    Jibu

    Zipo vizuri

    Jibu

Acha ujumbe

Meridianbet
Privacy Overview

This website uses cookies so that we can provide you with the best user experience possible. Cookie information is stored in your browser and performs functions such as recognising you when you return to our website and helping our team to understand which sections of the website you find most interesting and useful.