Bernard Morrison, winga mpya wa Klabu ya Simba rasmi atakipiga kwenye klabu hiyo baada ya Shirikisho la Soka Tanzania kumtambulisha kwamba ni mchezaji wa timu hiyo.

Agosti 30 kwenye kilele cha Wiki ya Mwananchi Yanga ilimtambuisha Morrison kuwa mmoja kati ya wachezaji wake 28 kwa kueleza kuwa mchezaji huyo kesi yake ipo Mahakama ya Kimataifa ya Usuluhishi wa Masuala ya Wachezaji,(Cas).
Mchezaji huyo pia Agosti 22 kilele cha Simba Day alitambulishwa kuwa mchezaji wa Simba na Agosti 30 jambo lililomfanya awe mchezaji pekee aliyetambulisha mara mbili ndani ya Uwanja Mkapa.
Morrison aliyekuwa na mvutano na mabosi wake hao wa zamani, alitajwa kwenye kilele cha Wiki ya Mwananchi kama mchezaji wa Yanga, akiwa jijini Arusha kukinukisha kwenye mechi ya Ngao ya Jamii ya timu yake mpya ya Simba iliyoishinda Namungo kwa mabao 2-0.

Lakini mashabiki wakiwa bado hawaamini kama nyota huyo aliyewapa raha msimu uiliopita kwa kuwatungua Simba katika mechi ya marudiano ya Ligi Kuu Bara, atasalia kikosini mwao, katika orodha ya usajili mpya ya TFF kwa msimu ujao jina lake limetokezea Simba kuonyesha ni mali yao rasmi sasa.
Ofisa habari wa TFF, Cliford Ndimbo, amesema kilichomfanya Morrison awe kwenye orodha ya Simba badala ya ile ya Yanga ni kwa kuzingatia maamuzi ya Kamati ya Sheria na Hadhi ya Wachezaji iliyomtambulisha kama mchezaji huru baada ya kusikiliza kesi iliyomhusisha Mghana huyo na Yanga.
SHINDA NA HI LO
Sasa hii ni rahisi zaidi kupata USHINDI! Unatabiri karata ipi ipo chini au juu, kisha unakusanya mkwanja wako.


Ester jackson
Yote heri mana safari bado inaendelea
Zeiyana
Merrison wakawaida tu simba waache habari za Morrison wazungunze na habari za kagere kumpiga kocha kichwa na alivyo komaa sijui hana ali gani uyo kocha
Fatina mfigi
Karibu msimbazi merrison acha na kekele za yanga!!
Caroline
Morrison hatukutaki yanga.kwanza ww ndo ulisababisha tukafungwa nne.msaliti mkubwa wewe
Elika
Wamuache morison aende anapopahitaji..morison ni wa simba tuu huko yanga hana anachokiitaji
magdalena
utopolo wanatapatapa na kujipa matumaini ya kuwa morissoni atarudi kwao waache tu kujipa matumaini ayo
Adelta
Maamuzi Ni yake mwenyewe @meridianbettz
Dorophina
Morrison yuda haende tu huko simba sisi hata hatumuhitaji tena
Mwanahamisi
Maamuzi ni yake mwenyewe
Mwajumah
Morrison ni mchezaji mzur sana karibu simba ila ule ujeuri wa zaman ulipokua yanga uwache ukouko kwa utopolo#Meridianbettz
felister
aende tu hatumtaki wala nini
Sauda
Morrison ni wa Simba tu
Ernest
Hapa hatutaki tena kusikia fyokofyoko za wazee wa kikapu aka Utopolo Fc, wajipange kivingine pia iwe fundisho kwa viongozi wa club hapa nchini kwenye kwenye Janja janja kuhusu mikataba ya wachezaji maana ilikuwa Aibu kubwa kwa Mchezaji mkubwa kama Morrison kupata kashfa kama hii wakati yeye ni Professional na anaelewa kazi yake, Viongozi wa Yanga na vilabu vingine vyote hapa Nchini Tanzania kuna kitu cha kujifunza Hapa.
Tatu
Yanga inamatatizo sana badala wajipange kwa ajili ya msimu ujao wao wanapoteza mda kwa mchezaji mmoja kama Morrison
Lydia Emmanuel Magoti
Vizuri Sana Morrison kuwa halari yasimba iyo ainaubishi mbona inaeleweka Kama Morrison Ni wasimba
Genia Sikaluzwe
Ahsant meridian kwa taarifa
Shafii
Habari njema kwa wana msimbazi.
Nasra
Hongera sana morrison
Sadick
Issue ya Morrison imeonyesha namna ambazo tunaendesha mambo yetu bila kufuata utaratibu#meridianbettz
JULIANA
Ndioooo ni mali ya mabingwa
Khadija
Karibu simba damu morrison hila umejua kuwakausha mashabiki koo#meridianbettz
Issa
Tff kama wanaleta ushabik kwenye hili swala la morrison wasubir wazee wa utopolo maamuz ya fifa kuhusu hili swala
Rose kapinga
Wanayanga lazima watoke mapovu,ila Morrison yupo unyamani atakiwasha balaa!!!
Hope mwaikuka
Bora wanna yanga watulie tumechoka na madai yao
Saupha mohamed
Karibu sana
rama
vizuri na ubora wake umeonekana
Shani
Ishu ya morrison itasumbua sana tff isimamie kwenye haki si kutoa maamuz sabab ya ushabik
Samiah
Karibu sanaaa
Sabrina
Kesi hii imeshikiliwa sana kiushabiki kuweni wapole hadi itakapo tolewa uamuzi
Rehema
Karibu sana
farida ahmadi
Morrison ni mchezaji mzuri Sana
Povel
Bm3 sheria imefuata mkondo wake
Amiri Kayera
Yanga wanajua Ila wanawaongopea mashabiki zao
Gabriel
Morrison hatukutaki yanga.kwanza ww ndo ulisababisha tukafungwa nne.msaliti mkubwa wewe
Tahiya
Wana yanga mmesikia iyoo
warda
Hadi raha
aisha
Simba wa wanajifariji