Thomas Tuchel: Christensen Alikuwa na Sababu ya Kujitoa

Kocha wa klabu ya Chelsea Thomas Tuchel amemkingia kifua beki wake Andreas Christensen kwa kusema kuwa kujiondoa kwake dakika za mwisho kwenye kikosi hicho kabla ya mchezo wa fainali ya FA Cup sio mara ya kwanza kwake mlinzi huyo alijihisi kutoweza kucheza msimu huu.

Andreas Christensen inaelewaka kuwa hakuwa majeruhi, na aliku kwenye mipango ya Thomas Tuchel kuwepo kwenye kikosi kilichopaswa kucheza dhidi ya Liverpool kwenye usiku wa jumamosi ndani ya dimba la  Wembley.

Thomas Tuchel
Thomas Tuchel

Tuchel siku ya jumatano alizungumza na kusema mchezaji huyo wa kimataifa wa Denmark alimwambia siku ya mchezo wa fainali hayuko tayari kucheza, alikuwa na sababu na itakuwa yao binafsi na siri.

“Lakini sio mara ya kwanza, kama unavyoona wiki iliyopita tulikuwa na baadhi ya matatizo sawa kama hili ndio maana hakuweza kucheza mara kwa mara.

“Tunadhani kwamba tulikuwa na maendelezo na maendeleo mazuri kwa sababu alicheza kwa nguvu kwenye mchezo dhidi ya leeds kabla ya fainali. 

“Lakini mazungumzo tuliyoyafanya inapaswa kuyaheshimu, na bila shaka tumeyaheshimisha na yeye nimsaada wetu.”


TENGENEZA FAIDA NA ZEUS ANCIENT FORTUNES

Una Kila sababu ya kufurahia wiki yako na kutengeneza mwaka huu uwe wa faida zaidi katika kasino zetu za mtandaoni za meridianbettz. Mchezo wa Zeus Ancient Fortunes unakuongoza kutekeleza hilo.

tetesi, Tetesi za Soka Barani Ulaya., Meridianbet

CHEZA HAPA

Acha ujumbe