Tyson Furry anamtaka Deontay Wilder ulingoni tena haraka iwezekanavyo. Furry anasema kuwa yeye hawezi kusubiri milele kwa kuwa ana vibarua kibao vya kumalizia kwenye ndondi.
Pambano la marudiano, ikiwa ni mechi ya tatu wawili hawa kupanda ulingoni ilikuwa inatarajiwa kuwa Desemba 19. Lakini kumekuwa na sintofahamu ya tarehe rasmi ya pambano hilo kutokana na mabadiliko kadhaa.
Furry tayari alikuwa ameshafanya makubaliano ya kupambana dhidi ya Anthony Joshua mwaka 2021. Lakini pia Dillan Whyte anajiandaa kupambana na mshindi wa pambano la Fury dhidi ya Wilder, na kwa mujibu wa promota Eddie Heran, Whyte ndiyo Kipaumbele.

Ili Furry aweze kupanda ulingoni na Whyte, anahitaji kuwa amemtandika Wilder, kisha hapo ataendelea na mipango ya kuwania taji dhidi ya Anthony Joshua.
White anahitaji kupambana na Alexander Povetkin Jumamosi, pambano la lazima kuwania taji la WBC Heavyweight ambalo Furry alilipata dhidi ya Wilder.
Kupitia ukurasa wake wa Twitter, Furry ameweka chapisho lenye picha yake akiwa anamtandika Wilder.
“Uko wapi mzee? Mda unaenda!! Sitaweza kusubiri milele!!! Kuna maandazi kibao kwenye daraja hili nahitaji kuyala kama kifungua kinywa” -Tyson Furry
Drops and Wins!
Umeijua hii? Ni promosheni kabambe ya ushindi kwenye Casino ya mtandaoni ya Meridianbet! Unaweza kushinda hadi Euro 2,000,000 leo.


Devotha
Tyson anatamba tu: asichoke kusubiri muda utafika na pambano litafanyika tu alafu akipigwa arudi tena kwenye ukurasa wake aseme
Gabriel
Kiukwel Tyson furry hamuwez kabisa Deontay Wilder kwan Kama ukibahatika gemu ya kwanza tuliona furry akipigwa Kama mtoto ila nilishangaa kuona mech ya pil upande wa wilder alionekana Kama hakuwa poa kabisa ila upande wangu kama gemu ikirudiwa tyson furry anapigwa
Povel
Mashabik wa masubwi tunasubir matanange kwa hamu kwl
Amiri Kayera
Litakua pamban zur san
Sabrina
Tunangoja kuona kuona pombano litakuaje
Theonestina
Kitakuwa bonge la pambano
Janeflora malisa
🔥🔥
David Pere
Kiukwel Tyson furry hamuwez kabisa Deontay Wilder kwan Kama ukibahatika gemu ya kwanza tuliona furry akipigwa Kama mtoto ila nilishangaa kuona mech ya pil upande wa wilder alionekana Kama hakuwa poa kabisa ila upande wangu kama gemu ikirudiwa tyson furry anapigwa
Fatuma kasomo
Patakua hapatoshi
Mwanahamisi
Patachimbika bila jembe
Ernest
Wapange mapema tumalize ubishi bhana
warda
Furry nae kujitapa amezidi ngoja siku apigwe ndo atakoma#Meridianbettz
Sauda
Tunasubiri mtanange
Nasra
👍👍
Ester jackson
Katika wapambanaji Naukubali sana Deontay Wilder mana Tyson anaongea sana angekutana kwanza na wilder ingependeza sana
Dorophina
Tyson najua atamuangusha mtu nausubiria kwa hamu mtanange huu
Mwajumah
Wapange mapema tumalize ubishi bhana#Meridianbettz
Khadija
Tunasubili huo mtanange kwa hamu#meridianbettz
felister
nasubiria kuona hilo pambano litakavyokua
Adelta
Mashabiki tunasubiri kwa ham tuone Nani zaidi@meridianbettz
Magdalena
tyson yupo makini sana namkubali
Zeiyana
Bado hajapatika mbadala wa Tyson
Samira
Huu mtanange utakua ni balaa tunausubiri kwa hamu
Hope mwaikuka
👀
Sadick
Sikutarajia kama Wilder angepigwa vibaya pambano la pili na Tyson Fury anaonyesha ana usongo wa kuwa bingwa wa heavy weight duniani#meridianbettz
Furahav
Mchezo wa ngumi naupendaga sana.
Issa
Furry anampania sana huyu mtu lakin mwisho anaangukia pua
Shafii
Pamba
aisha
Sipati picha maana tunasubili pambano hilo kwa hamu
Lydia Emmanuel Magoti
Tunausubili mtanange huo kwahamu patakuwa apatoshi hapo