Waingereza Ghali kwa Sasa

Kwa mara ya kwanza kulinganisha na kitambo inaonekana kuna mwanga katika soka kwa taifa la Uingereza. Kwa sasa wamekuwa wakifanya vizuri kitu ambacho kinaweza kuwafanya kurejea kwenye aina ya soka ambalo kila mmoja atavutiwa nalo kwa kiasi kikubwa sana.

Hisia za kila mmoja ziliweza kurudi mahala pake ikiwa kihistoria ni tangu miaka ya 1990 ambapo walifanya vizuri ndipo walitakiwa wakae chini na kujitathmini juu ya mzizi uliokuwa ukiwatafuna mara nyingi hadi kushindwa kufanya vizuri kwenye michuano mikubwa. Kwa sasa wamekuja kivingine na wanaonekana kabisa kudhamiria kile wanachokifanya.

Tangu Gareth Southgate akichukue kikosi hicho kumeshuhudiwa mabadiliko makubwa sana upande wa soka la Uingereza huku wakiweza kufanya vizuri hata katika fainali za kombe la dunia zilizofanyika Urusi kwa kutinga hatua ya nusu fainali ya michuano hiyo. Jambo hilo liliwafurahisha wengi kutokana na misingi waliyokuwa nayo.

Lakini kinachowapa nguvu Waingereza hao ni kile kitendo cha wao kufanya vizuri kwenye michuano hiyo na humo ndimo imani yao kubwa ilimo. Pamoja na hilo wanafurahia uhalisia wa kile kinachofanywa na wachezaji wao ndani ya ligi hiyo na nje pia kwamba ni jambo kubwa sana na lenye kujivunia kwa taifa hilo. Baadhi ya wachezaji wanaofanya vizuri na kuwa na thamani kubwa ni:

Jordan Pickford, baada ya kuonesha kiwango cha kuvutia amejichanjia namba ya kudumu kikosini kwa amani kabisa. Anafanya vizuri ndani ya Everton lakini kuna baadhi ya vitu anavifanya vinatokea kugharimu timu yake. Japo mengi yametokea katika ngazi ya klabu. Thamani yake ni £40.5m.

Harry Maguire, mlinzi huyo amekuwa aking’aa sana katika nyanja mbalimbali za kiulinzi jambo ambalo linamfanya kuwa mchezaji wa aina yake. Thamani ya mchezaji huyu ni £40.5m; uwezo wake huo unawavutia United washawishike kutuma ofa zao.

John Stones, uwezo wake umekuwa kwa kasi sana tofauti na alivyokuwa akidhaniwa mara ya kwanza kwamba asingeweza kuwa na msaada mkubwa kwenye kikosi cha taifa na klabu yake. Kwa sasa thamani yake ipo kwenye kiwango cha £54m.

Mbali na hao kuna wengine thamani yao ipo juu sana kama vile Sancho mwenye thamani ya £72m, Rashford  £72m, Dele Alli ambaye thamani yake ni £90m, Raheem Sterling  £108m anayefanya vitu vya pekee na klabu yake ya Man City, pia uwepo wa watu kama Harry Kane ambaye amekuwa mhimili mkubwa sana kwa kikosi cha taifa hilo na thamani yake inatua kwenye kiasi cha  £135m.

5 Komentara

    Waingereza wako vizuri.

    Jibu

    Sana walijiandaa vilivyo

    Jibu

    Waingereza wanajua kufanya marketing ya wachezaji wao. Wanajihesabu ni bora kuliko wengine duniani#meridianbettz

    Jibu

    Waingereza wanajipandisha dhaman Ila uwanjan hakun lolote

    Jibu

Acha ujumbe

Meridianbet
Privacy Overview

This website uses cookies so that we can provide you with the best user experience possible. Cookie information is stored in your browser and performs functions such as recognising you when you return to our website and helping our team to understand which sections of the website you find most interesting and useful.