Ikiwa lile sekeseke la klabu ya ligi kuu ya Uingereza, Newcastle United kunuliwa na mabilionea wa Saudi Arabia linakaribia kufikia mwisho, ni suala la muda tu kabla Newcastle hawajawa kama Chelsea ya Roman Abrahmovich na Manchester City ya Sheikh Mansour.
Bilionea wa Newcastle, Ashley yu mbioni kuachia klabu hiyo kwa mfuko wa Uwekezaji wa Saudi Arabia (PIF) ambao unaongozwa na mwana mfalme Prince Mohamed Bin Salman kwa bei ya paundi milioni 300.
Ikiwa dili hilo litafanikiwa basi tujiandae kuishuhudia Newcastle yenye misuli ya kutosha kushindana katika mbio za ubingwa wa ligi kuu hata kushiriki mashindano makubwa ya Ulaya hasa kutokana na uwekezaji utakaofanywa na bilionea huyo wa Saudia. Kabla hata dili lenyewe halijakamilika kumekua na tetesi za wamiliki hao kutaka kumleta klabuni hapo aliyekua kocha wa Tottenham Mauricio Pochettino. Nyota wa zamani wa Newcastle Mick Martin alinukuliwa na gazeti maarufu la michezo la Uingereza, the Express akimzungumzia kocha huyo, “Pochettino anawajua wachezaji wazuri, anaijua America ya Kusini na Ulaya pia. Ni kocha bora kwa sasa.”
Kama hiyo haitoshi, ili kuimarisha kikosi hicho cha Newcastle United na kukifanya kuwa bora wamiliki hao wameonesha kuhusishwa na wachezaji wafuatao:
Phillipe Coutinho. Watakaokuwa mabosi wapya wa Newcastle wanatajwa kuhusishwa na nyota huyo wa Barcelona anayekipiga kwa mkopo katika timu ya Bayern Munich ya Ujerumani. Kama dili hilo la ununuzi wa timu ya Newcastle United likitimia basi itawalazimu kutoa kitita cha pauni milioni 70 au zaidi ili kupata saini ya nyota huyo.
Nafasi ya mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 27 inaonekana kuwa yenye mashaka hivyo anaona ni bora aende sehemu nyingine kutafuta chabgamoto mpya, hakubaliani kuwa mchezaji wa ‘mkopo’. Timu nyingine ambayo itachuana na Newcastle United kwa mchezaji ni Chelsea ya Uingereza.
Antoine Griezmann ni mchezaji mwingine ambaye anatajwa kuwa anaweza kutua St. James’ Park kama mambo yakienda sawa. Jarida la michezo la Sport Mediaset limeripoti kuwa wamiliki wapya wa Newcastle wanavutiwa na nyota huyo wa Barcelona na kuhusu kumnunua ni suala la muda tu kwani pesa kwao sio tatizo.
Moussa Dembele wa Lyon ya Ufaransa ni mchezaji mwingine matata anaetajwa na kuangaliwa sana na mabosi hao. Klabu hiyo ya Newcastle imekua ikihaha kuhitaji huduma ya nyota huyo kila mara na mara zote hizo dili hilo limekua likikwama kutokana na Lyon kuhitaji pesa nyingi ili wamuachie nyota huyo. Kwa ujio wa wamiliki wapya ni wazi kuwa dili hilo linaelekea kutimia kwani wao sio mabahili kama bilionea Ashley ambaye ndiyo mmiliki wa sasa wa The Magpies.
Kylian Mbappe ni mchezaji anaetajwa sana na mashabiki wa Newcastle United lakini sio na viongozi wala wamiliki hao wapya. Mashabiki hao wa The Magpies wanaamini pesa ndiyo kila kitu, kwamba pesa ikiwekwa mezani tu unaweza kufanya kila kitu katika soka. Umtoe Mbappe PSG na kumleta Newcastle, bila shaka wanaamini hata Messi wa Barcelona wataweza kumchukua dili hilo likitimia.
Kwa hili la Mbappe sioni kama kuna uwezekano mkubwa sana wa kutimia kwani kwa umri wa Mbappe ni umri ambao hahitaji kwenda katika timu ambayo ndiyo kwanza inajijenga, anahitaji timu ambayo tayari imeishajijenga ili apate mafanikio katika soka akiwa bado mdogo. Ila wanasema kuwa katika mchezo wa soka lolote linaweza kutokea, tuuachie muda uamue.
John McGinn. Sio tu wachezaji wa nje ya ligi ya EPL tu wanaotajwa, kuna wachezaji kadhaa wa vilabu vya ligi kuu ambao wanatajwa kuhusishwa na Newcastle iwapo dili hilo litakamilika. The Magpies watatakiwa kutoa kiasi cha £20 ili kupata saini ya nyota huyo wa Aston Villa, lakini kikwazo kingine watakachokumbana nacho katika dili hilo ni Manchester United ambao nao wameonesha kuvutiwa na mchezaji huyo.
Dwight McNeil. Moja kati ya timu Zilizotoa ushindani ligi kuu ya Uingereza ni Burnley ambao hawakupewa nafasi kabisa mwanzoni mwa msimu, lakini walichokifanya mpaka sasa sio cha kupotezewa. Burnley mpaka ligi inasimama walikua nafasi ya kumi katika msimamo wa EPL, mafanikio yao yamechagizwa na uwekezaji uliofanywa na mmiliki wa klabu hiyo tajiri Mike Garlick na juhudi binafsi za wachezaji.
Ukitaja mafanikio ya klabu ya Burnley huwezi kuacha kutaja jina la winga machachari wa timu hiyo Dwight McNeil. Mchezaji huyo ni lulu ya timu hiyo kutokana na kiwango chake kinachokua siku baada ya siku. Kama Newcastle wakifanikiwa kupata saini ya nyota huyu watakua wamefanya usajili mkubwa na muhimu kwa maendeleo ya timu yao.
Tuwaombee mabilionea hao wafanikiwe katika dili lao la kuinunua klabu hiyo ili hizo hela zao za mafuta zipate pa kutumika, mana mara nyingine kuwa na pesa na huna namna ya kuzitumia ni sawa tu na hauna.


Lombo
Asante meridianbet kwa habari zenu
Asha
Itakuwa poa sana
Rehema Dickson
Kumbe Newcastle inauzwa sikulijua hili asante kwa taarifa meridian
Swai
Now Newcastle watakuwa wacharooo
Mwanaidi
Habari za uhakika za michezo tunazipata kwenu meridian bet
Ester mmakasa
Wachezaji wote ni wazoefu katika soka wanafaa kununuliwa.
aisha
mmetisha sana meridianbet kwa habari mzuri
mathayo sonje
Tumuombee afanikiwe kuinunua hiyo klab maana itaongeza ushindano mkubwa kwenye ligi maana ,MBAPE, McNEIL, McGINN, NDEMBELE, na GRIEZMANN Sio poa, hii timu italeta upinzan mkubwa EPL.
Tahiya
Newcastle watakuwa wameramba dume
Evaluziga
Mnatisha meridian kwa kazi nzuri
Hopemwaikux
Hii iko poa sana
Frank Patrick
Hizi ni taarifa za furaha kabisa kwa Mh.Rais mstaafu Jakaya Mrisho Kikwete (uncle) na Newcastle yake
Shafii
Newcastal itakua Moto wa kuotea mbali
Tatu
Hii team itakuwa si ya kitoto ikinunuliwa
Lydia Emmanuel Magoti
Itakuwa vizuri sana
Salma
Hii safi
Povel
Tuombe wafanikiwe jambo hlo ili epl iwe na ushandi Zaid kwn hv Sasa tuna vita tatu ya kushuka daraja na vita ya ubingwa na top four na Kama watafanikiwah kutakuwah na vita ya top ten ya epl itakuwa tamu Zaid Asante kwa habar ya kimichezo
hamidu
tusubili tuone.. kama timu itanunuliwa watakuwa ni timu ya ushindani katika epl & ulimwenguni
Kenani
Wapate mtu anaejua kiwekeza kwa kutengeneza team ili ilud kwa ujio wa kasi
David Pere
Wainunue waiboreshe ili waweze kuleta uponzani kwenye Epl
SADICK
Wamiliki wapya wanaonekana wamejipanga, tutarajie makubwa. Asante#meridianbettz
felister
Newcastle watakua wameokota embe dodo kwny muarubain
Theckla
Itakuwa habari njema kwa mashabiki wa Newcastle
mwakalosi
hii ni habali mbaya kwa skysport na Bt sport
Fatina
Asanteh kwa taarifa
Antony Luseno
💰 talks
Elika
Ukiwa na pesa utaitwa majina mengi..hapo pesa tu inaongea
Adelta
Ni habari njema Asante meridian
Furahav
Itakuwa hatar sana.
Ernest Kimeru
Safi sana, Newcastle itarudisha heshima yake kwenye ulimwengu wa soka!!!!!
Dorophina
Mnatupatia habari muhimu sana meridian
Warda
Si wakuje Manchester Tu🤸🏻♂️
Mariam
Hii itakuwa vizur
Njiku
Newcastle ipo sokoni duuh
Emnmy cleopa
Itakuwa vizur sana
khadija
itakuwa poa
Rehema
Asante meridianbet kwa habari njema
Agness
Mnatutaarifu mambo mazuri asante meridian
amon
ligi ya england itakuwa na mvuto zaid mana wachezaji watakao chukuliwa n nitishio katika ligi zao
Isaya massawe
Mnatuhabarisha sana meridianbet
Isaya massawe
Waarabu wana jeuri ya pesa
Nasra
Pesa Ipo lakn
Daniel
If this deal is approved they will spend so much. Good article @meridianbettz
Neema hassan
Messi kuhama Barcelona watasubiri saana..
Samiah
Wachezaji wote wapo sawa
Gabriel
Good news 👍
Ester jackson
Asante kwa habari nzuri
Julieth Boniface
Habari nzur safi sana
Neema juma
Kumbee asante meridianbet kutujuzaa hii habari
Mwajuma
Mambo yatakuwa moto sana
David pere
Wnaonekana Wana pesa sna Hawa jamaa