Mashirikisho ya ligi mbalimbali za ulaya zimelitaka shirikisho la soka barani ulaya UEFA kuitia tena upya mpango wake wa kuongeza michezo zaidi ya ligi ya mabingwa ulaya na kusaidia timu kuweza kufuzu michuano hiyo kutokana na ubora wao wa mashindano yaliopita.
Bodi za ligi mbalimbali barani ulaya zimeunda kundi ambalo wamepanga kupinga kwa sababu mpango huo utawapendelea vilabu vikubwa tu, na wamewambia UEFA kuwa timu zote zinazopaswa kufuzu ni lazima zifanikiwe kufuzu kwenye ligi za nchi kwao.
“Kuongezeka kwa michezo kwa zaidi ya 50% kutaumiza timu nyingi kwa sehemu kubwa na kunufaisha timu chache” mwenyekiti wa shirikisho la ligi za ulaya Claus Thomsenalizungumza baada ya mkutano wa Istanbul. “Tunapswa kuwa na idadi ndongo ya mzungukuko.”
UEFA imepanga kuongeza idadi ya timu kutoka idadi ya timu ya sasa 30 hadi 36, huku kukiwa na timu zingine ambazo zinatokwa kwenye ligi tano kubwa ulaya ambazo zimeshindwa kufanya vizuri kwenye ligi zao na kukosa nafasi ya kushiriki mashindano hayo.
Una Kila sababu ya kufurahia wiki yako na kutengeneza mwaka huu uwe wa faida zaidi katika kasino zetu za mtandaoni za meridianbettz. Mchezo wa Zeus Ancient Fortunes unakuongoza kutekeleza hilo.