Mshambuliaji wa timu ya taifa ya Brazil Neymar Jr atakosekana kwenye michezo iliobakia ya hatua ya makundi kwenye michuano ya kombe la dunia baada ya kupata majeraha.
Staa huyo alipata majeraha katika mchezo wao dhidi ya timu ya taifa ya Serbia ambapo Brazil ilishinda mabao mawili kwa bila, Lakini staa huyo alipata majeraha ya enka ambayo yamekua yakimsumbua mara kwa mara.
Taarifa kutoka kambi ya timu ya taifa ya Brazil inaeleza kua Neymar atakosekana kwenye michezo ya hatua ya makundi iliobaki ambayo ni dhidi ya Uswisi na timu ya taifa ya Cameroon katika mchezo wa mwisho.
Hii inakua mara ya tatu kwa staa huyo kuumia akiwa anaitumikia timu ya taifa kwani mwaka 2014 kwenye michuano ya kombe la dunia iliofanyika Brazil alipata majeraha katika hatua ya robo fainali dhidi ya Colombia, Pia kuelekea michuano ya Copa America mwaka 2021 pia alipata majeraha na kushindwa kushiriki michuano hiyo.
Kocha wa timu ya taifa ya Brazil Tite ameeleza licha ya Neymar kupata majeraha na kukosa michezo ya hatua ya makundi iliobakia, Lakini amewatoa hofu mashabiki wa timu hiyo kua staa huyo ataendelea kucheza michuano hiyo kwenye hatua zinazofuata.

Je wewe hucheza Kasino Mtandaoni na umekuwa ukijiuliza ni mchezo gani rahisi na mzuri kwa ushindi? Basi Usihangaike Aviator ni rahisi zaidi kucheza na kushinda, kingine cha zaidi ni kwamba Aviator Bonanza imerudi tena Cheza zaidi ujiweke kwenye nafasi ya kushinda Samsung A23.

