Kiungo wa klabu ya Yanga na timu ya taifa ya Tanzania Feisal Salum Toto atakosekana katika mchezo wa kesho dhidi ya klabu ya Mbeya city kutoka mkoani Mbeya.
Kiungo atakosekana katika mchezo huo kutokana na kupata kadi tatu za njano jambo ambalo kikanuni linamfanya kukosa mchezo huo utakaopigwa katika dimba la Benjamin Wiliam Mkapa siku ya kesho.
Kiungo Feisal ni miongoni mwa wachezaji tegemezi wa klabu ya Yanga kwasasa kwani namba zake zinaonesha namna alivyo na umuhimu katika timu hiyo kwani mpaka sasa ameshaweka mabao manne kimiani kwenye ligi kuu.
Kiungo huyo fundi atakosekana kwenye mchezo huo lakini taarifa njema kwa mashabiki wa klabu hiyo ni kurejea kwa kiungo mwingine mwenye ubora klabuni hapo Aziz Ki ambaye alikua mapumzikoni nchini kwao Burkina Faso.
Vilevile kocha msaidizi wa klabu hiyo Cedric Kaze ameongea kuelekea mchezo dhidi ya Mbeya City na kueleza wanaenda kucheza mchezo kutafuta alama tatu lakini akionya hawachezi ili kulinda rekodi yao kutokufungwa.

Je wewe hucheza Kasino Mtandaoni na umekuwa ukijiuliza ni mchezo gani rahisi na mzuri kwa ushindi? Basi Usihangaike Aviator ni rahisi zaidi kucheza na kushinda, kingine cha zaidi ni kwamba Aviator Bonanza imerudi tena Cheza zaidi ujiweke kwenye nafasi ya kushinda Samsung A23.

