Kessy kutimkia Ruvu Shooting

HASSAN Kessy beki wa zamani wa Yanga na Simba ambaye msimu wa 2021/22 alikuwa ni mali ya KMC anatajwa kumalizana na mabosi wa Ruvu Shooting.

Kessy atajiunga na Ruvu Shooting akiwa ni mchezaji huru baada ya KMC kuweza kumshukuru kwa mchango wake ambao aliweza kuutoa kwa msimu uliopita.

Ofisa Habari wa KMC,Christina Mwagala amesema kuwa Kessy wao wameshamalizana naye labda kwa wahusika wenyewe.

“Kuhusu Kessy,(Hassan) sisi tumeshamalizana naye tayari sijui labda kwa huko,” Julai 20,KMC walimuaga rasmi beki huyo.
Kwa upande wa Ruvu Shooting,Ofisa Habari Masau Bwire alisema kuwa mipango ikiwa tayari kila kitu kitawekwa wazi.

Acha ujumbe

Meridianbet
Privacy Overview

This website uses cookies so that we can provide you with the best user experience possible. Cookie information is stored in your browser and performs functions such as recognising you when you return to our website and helping our team to understand which sections of the website you find most interesting and useful.