Bosi Yanga Afunguka Alivyomsajili Aziz Ki

RAIS wa klabu ya Yanga, Eng. Hersi Said amefunguka kuwa hawakutumia gharama nyingi kumleta mchezaji huyo bali walitumia akili kubwa.

Aziz Ki ni miongoni mwa wachezaji watano waliosajiliwa kwenye kikosi cha Yanga katika dirisha kubwa la usajili ambalo linatarajiwa kufungwa Agosti 30, mwaka huu.

Akizungumzia hilo, Hersi amesema kuwa “Haijatumika hela nyingi kumpata Aziz Ki kama watu wanavyofikiria ni mikakati ambayo niliitumia ili kuweza kumpata mchezaji.

“Nilitengeneza mahusiano muda mrefu pia kuna ujanja ulitumika hata kuingia kwenye levo ya familia hata mama yake alikubali kumleta mtoto wake kucheza kwenye klabu yetu, pia alipata uthibitisho kutoka kwa mchezaji wetu Yacouba.

“Alikuwa amepewa ofa kubwa zaidi kuliko hapa Tanzania pia kulikuwa na klabu ya hapa nchini ilipeleka ofa kubwa zaidi yetu lakini alikubali kuja hapa kutokana na mazingira mazuri.”

Acha ujumbe

Meridianbet
Privacy Overview

This website uses cookies so that we can provide you with the best user experience possible. Cookie information is stored in your browser and performs functions such as recognising you when you return to our website and helping our team to understand which sections of the website you find most interesting and useful.