Sergio Aguero Amuonya Nicolas Otamendi

Nyota wa zamani wa kimataifa wa Argentina Sergio Aguero amemtania mlinzi Nicolas Otamendi kwa kumkanya kutokumchezea vibaya nyota wa timu ya taifa ya Argentina Leo Messi kwa sababu anahitajika kwenye michezo ya kombe la dunia mwaka huu nchini Qatar.

Messi kwa sasa anaichezea timu ya PSG huku Otamendi yeye akiichezea Benfica amba po kwenye mashindano ya Ulaya wamepangwa kundi moja ambapo wanatarajia kukutana kwenye michezo miwili ya kundi H, huku kikiwa na timu za PSG, Benfica, Juventus na Maccabi Haifa.

Sergio Aguero akizungumza kwenye Channel yake ya Twitch, alimuomba Otamendi asimfanyie madhambi nyota huyo watakapo kutana kwenye michezo ya klabu bingwa barani ulaya kwani wanamtegemea kwenye michezo ya kombe la dunia.

“PSG, Juventus, Benfica, Otamendi atakwenda kuwapiga watu viatu. Otamendi yupo Benfica , kwaiyo ataanza kufanya vurugu zake na atakutana na messi. Usimumize messi , kwa sababu nitakuua. Kombe la dunia linakuja, Ota.’

 

 

 

Acha ujumbe

Meridianbet
Privacy Overview

This website uses cookies so that we can provide you with the best user experience possible. Cookie information is stored in your browser and performs functions such as recognising you when you return to our website and helping our team to understand which sections of the website you find most interesting and useful.