Matokeo ya Mechi Bundesliga

Bayer Leverkusen v Schlake 04

Bayer Leverkusen wamelazimishwa sare ya 1-1 na wachovu Schalke 04. Matokeo hayo yanawafanya Leverkusen wafikishe alama 57 huku wakiwa nafasi ya nne katika msimamo wa Bundesliga huku wakibakiwa na michezo minne ya ligi hiyo.

Kwa upande wa Schlake 04 wao matokeo hayo yanawafanya waweke rekodi mbaya kwa timu yao kwa kutokushinda katika michezo 13 mfululizo ya Bundesliga kila mara wakiwa na sababu tofauti tofauti lakini kwa mechi hii lawama nyingi zitamuendea mlinzi wao Juan Miranda aliyejifunga dakika za jioni kabisa za mechi hiyo.

Schlake 04 walikuwa wanaelekea kushinda mechi hii kutokana na goli walilolipata mapema mwanzoni mwa kipindi cha pili. Hali ilibadilika katika dakika ya 81 baada ya Miranda kujifunga na kufanya mchezo huo uishe kwa sare ya 1-1.

Mainz v Augsburg

Pamoja na ushindi wa ugenini wa goli moja bila, Augsburg bado wapo katika hatari ya kushuka daraja. Hatari hiyo ni kubwa zaidi kwa Mainz waliokubali kipigo hicho cha goli 1-0 katika uwanja wao wa nyumbani. Matokeo hayo yanawapeleka Augsburg nafasi ya 13 ya msimamo wakiwa na alama 35 huku yakiwaacha Mainz katika nafasi ya 15 na alama zao 31.

Goli pekee la Augsburg katika mchezo huo lilifungwa na Florian Niederechne katika dakika ya kwanza tu!

Mpaka sasa, Bayern Munich wanaongoza msimamo wa ligi hiyo wakiwa na alama 73. Borussia Dortmund wanafuatia na alama zao 66. Kama Bayern wakishinda mechi yao ya Jumanne ya June 16 dhidi ya Werdee Bremen watafikisha jumla ya alama 76 hivyo ktawazwa mabingwa wa Bundesliga kwa mara ya tisa mfululizo!

43 Komentara

    Uku nako bundesliga kulinoga Sana ingawa kulikuwa kugumu kidogo

    Jibu

    Hii ndohabariii tunazozitakaaa kwa kweli

    Jibu

    Hapo ndio unajua nani kapanda kwenye msimamo wa ligi

    Jibu

    Asanteni kwa taarifa za matokeo meridian

    Jibu

    Kila lakheri Bayern ,mungu awapiganie mfanye vizuri .

    Jibu

    safi Bayern munich

    Jibu

    Bayern munich hongeren sana endeleeni vizuri#meridianbettz

    Jibu

    Kweli mpira hauna mwenyewe.

    Jibu

    Bayern munich bingwa

    Jibu

    Noma sana kwel mpira dakika 90s

    Jibu

    Daaah..!kweli mpira hauna mwenyew

    Jibu

    Asante kwa taarifa#meridianbettz

    Jibu

    Mainz wameniangusha sana #Meridianbettz

    Jibu

    Matokeo sioazuri Sana kwa sisi wazee wa kutafuta pesaa

    Jibu

    Liverkusen game ilikuwa ngumu sana kwao 04 walikaza sana

    Jibu

    Bayern Munich noma

    Jibu

    Dhaa wameniangusha mpaka mkeka wng umekufa

    Jibu

    Kila la kheri bayern

    Jibu

    habar mzur

    Jibu

    Habar nzuri

    Jibu

    Mtanange ulikuwa wa kibabe hatar

    Jibu

    Kwa ligi hii adi sasa bingwa ashajulikana

    Jibu

    Asante meridian Kwa taarifa

    Jibu

    Bayern mkali nilijua tuu kwamba atashinda

    Jibu

    Duu kweri mpira dakika 90 izozingine wanajua waho

    Jibu

    Asante kwa taarifa # meridianbet

    Jibu

    Dah jamvi langu limechanikah kikatil sana thnks meridian bet tz kwa update

    Jibu

    Leverkusen amenikera sana amechana mkeka wangu

    Jibu

    Habari mzuri

    Jibu

    💪💪 bayern

    Jibu

    Munich wanatisha

    Jibu

    Asante kwa taarifa

    Jibu

    Hongera kwa mechi zote zilizopata ushindi

    Jibu

    Munichi niwakali sanaaa

    Jibu

    Asanten kwa kutujuza

    Jibu

    duuh mpila hauna mazoea#meridianbettz

    Jibu

    Bayern Munich jembee

    Jibu

    Asante kwa taarifa

    Jibu

    Habari nzuri

    Jibu

    Bayern wanatisha sana msimu huu

    Jibu

    Bayern Munich jeshii hanajua Sana mpira

    Jibu

    Good

    Jibu

Acha ujumbe

Meridianbet
Privacy Overview

This website uses cookies so that we can provide you with the best user experience possible. Cookie information is stored in your browser and performs functions such as recognising you when you return to our website and helping our team to understand which sections of the website you find most interesting and useful.