Frank Lampard Matatani Kwa Mara Nyingine.

Kocha wa Chelsea, Frank Lampard anaendelea kuwa matatani kutokana na matokeo mabovu ya kikosi chake.

Hii ni baada ya Chelsea kupoteza mchezo wa 5 kati ya 8 waliyocheza kwa siku za karibuni. The Blues walikuwa uwanjani jana usiku kupambana na Leicester City pale King Power Stadium.

Frank Lampard alishuhudia vijana wake wakiambulia kipigo cha magoli 2-0 dhidi ya vijana wa Brendan Rodgers. Kupoteza mchezo dhidi ya Leicester, kunaweka rehani kibarua cha kocha huyo ambaye kwa muda sasa amekuwa akilaumiwa kwa kushindwa kukiongoza kikosi hicho.

Magoli ya Wilfred Ndidi na James Maddison yawapa ushindi Leicester City vs Chelsea.

Frank Lampard alipatiwa kiasi kikubwa cha fedha kwa ajili ya kufanya usajili na kuijenga upya Chelsea kwa ajili ya msimu huu. Mambo yanaendelea kuwa mabaya siku baada ya siku na sasa The Blues wanaporomoka mpaka nafasi ya 8 kwenye msimamo wa EPL.

Akizungumzia mustakabali wa kibarua chake ndani ya klabu hiyo, Lampard alisema “sina uwezo wa kuamua hilo. Nimekuwa nikiulizwa hili swali kwa wiki kadhaa sasa. Ninaelewa ni kwanini, ni matarajio ya klabu kama ni sawa au sio sawa.

“Niliichukua hii kazi nikijua kutakuwa na kipindi kigumu kutokana na kuwa na timu ambayo haipotayari kwa mashindano. Tulifungiwa (kusajili), tunawachezaji wadogo, tumesajili wachezaji wapya ambao tunaona wanajitahidi kuzoea mazingira. 

“Tunachoweza kukifanya kwa sasa ni kuendelea kupambana.”


USHINDI UPI NI MKUBWA KWAKO, £2,000,000? 🤑

Pokea mualiko wa Meridianbet na Pragmatic Play kutengeneza mkwanja kwenye kasino ya mtandaoni sasa. Jiunge sasa kupata ishindi huu.

INGIA MCHEZONI

14 Komentara

    Nadhani bado Abrahmovich ana imani nae lkn kama hali hii itaendelea mechi 2 au 3 zijazo atatupiwa virago

    Jibu

    Chelsea Bado wanakibarua kigumu

    Jibu

    Pole sana Frank

    Jibu

    Lampard ana kazi kubwa ya kukipanga vyema kikosi chake

    Jibu

    Lampard anazingua sana na kikosi chake

    Jibu

    Lampard sijui anakwama wapi

    Jibu

    Had huruma

    Jibu

    Lampard Wana kazi kubwa

    Jibu

    Sijui itakuaje

    Jibu

    lampard kazi anayo

    Jibu

    Jamani lampard!!!!!!.

    Jibu

    Lampard tuliza mshono

    Jibu

    Ilipofikia Lampard ndani ya hizi siku chache tutasikia jambo lake, Ameshindwa kuvaa Viatu ndani ya Chelsea mbali na usajili mkubwa uliofanywa na Chelsea, Sio kwa Mfumo wala Mbinu Lampard amegonga Mwamba

    Jibu

    Kawaida tu atakaa sawa

    Jibu

Acha ujumbe

Meridianbet
Privacy Overview

This website uses cookies so that we can provide you with the best user experience possible. Cookie information is stored in your browser and performs functions such as recognising you when you return to our website and helping our team to understand which sections of the website you find most interesting and useful.