Pep Guardiola anasema ana ndoto za kuiga utulivu wa David Moyes ‘kama Buddha’ wakati Manchester City inajiandaa kutoana jasho na West Ham siku ya Jumamosi.
Moyes amerejea katika EPL baada ya kuvifundisha vilabu kama Manchester United, Real Sociedad na Sunderland na kuwarudisha Hammers kwenye kiwango thabiti kitu kilichoonekana kuwa kigumu kwa soka la Ulaya.
Guardiola alimsifu Moyes kwa maisha yake marefu katika ukufunzi na, kinyume na baadhi ya taarifa zake hapo awali, alipendekeza angependa kuwa na kazi ndefu kama hiyo.
Guardiola alisema: “David Moyes – nampenda mtu wa aina hii, kama Roy Hodgson. Wamekuwa na muda mrefu sana kwenye soka. Ningependa kuwa kocha kwa miaka mingi na nina shauku hii ya kuwa meneja na kufanya kazi hiyo.
“Ana uzoefu mwingi. Ninaota siku moja kufika katika nafasi hii, ambapo kila kitu ni shwari. Wanaishi kama maisha ya Buddha – katika wakati mzuri na mbaya wanakuwa watulivu.
“Daima ananijali. Siwezi kusahau mchezo wangu wa kwanza kwenye Ligi Kuu ilikuwa dhidi ya Sunderland. Alikuwa meneja huko na alikuwa mwema sana, alinipa ushauri kuhusu Ligi Kuu.
BusttheBank ni sloti inayokupa Mkwanja wa kutosha. Ndio, hii ni sloti inayokupa faida ya hadi mara kibao ya dau lako. Ni Meridianbettz pekee utakapoweza kupata burudani hii.



Rahma
Asante kwa taalifa
Venerose
Asanteni kwa makala
Caroline
Kila mtu na uwezo wake
Mwanahamisi
Safi
Adelta
Hawawezi kufanya kila mtu na uwezo wake
Lydia Emmanuel Magoti
Kila mtu na kiwango chake
Fatina mfingi
Kila m2 na nafasi yake
neema hassan
Asante kwa taarifa#meridianbettz
Sarah
Kila mtu nauwezo wake
Hopemwaikuka
Mmh
warda
Guardiola anaanza sifa kama klopp