Tetesi zinasema, Liverpool wanavutiwa na winga wa Arsenal na England Bukayo Saka, 20, ambaye kandarasi yake huko Emirates inamalizika 2024.
Liverpool pia wametoa ofa ya mkataba kwa kiungo wa kati wa AC Milan wa Ivory Coast Franck Kessie, 25, ambaye mkataba wake San Siro unakamilika mwishoni mwa msimu huu.
Tetesi zinasema, Barcelona wanataka kumsajili beki wa Manchester City na Uhispania Aymeric Laporte mwenye umri wa miaka 27 msimu ujao.

Newcastle wanakaribia kumnunua mlinzi wa Lille Mholanzi aliyekadiriwa kuwa na thamani ya pauni milioni 30 Sven Botman, 21, kama sehemu muhimu ya biashara yao ya uhamisho wa Januari.
The Magpies pia wanamfuatilia kiungo wa Juventus kutoka Wales Aaron Ramsey, 31, huku West Ham na Everton pia wakimtaka mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 31.
Tetesi zinasema, Newcastle wameweka ofa ya kandarasi ya kubwa kwa winga wa Barcelona ambaye hana utulivu Ousmane Dembele, 24.
Chelsea wanakaribia kumnunua kiungo wa kati wa Monaco Mfaransa Aurelien Tchouameni, 21, ambaye anaweza kuwa chaguo nafuu kuliko nyota wa West Ham na England Declan Rice, 22.

Lyon wamekataa jaribio la Chelsea la kutaka kumuita beki wa kushoto wa Italia Emerson Palmieri, 27, ambaye yuko kwa mkopo katika klabu hiyo ya Ligue 1.
Tetesi zinasema, Leeds wanataka kumsajili mshambuliaji wa Argentina, Giovanni Simeone, 26, ambaye kwa sasa yuko kwa mkopo Verona kutoka Cagliari, majira ya joto.
Barcelona wamemfanya mshambuliaji wa zamani wa Chelsea, Alvaro Morata, 29, ambaye kwa sasa yuko Juventus kwa mkopo kutoka Atletico Madrid, kuwa lengo lao kuu la Januari.
Unaanzaje siku yako katika msimu huu wa sikukuu, mchongo upo meridianbet kasino. Sloti pendwa ya Sahara Richies inaweza kukufanya ukawa milionea katika kufunga mwaka huu, Jiunge na ufurahie kasino maridhawa kutoka nyumba ya mabingwa.

CHEZA HAPA

