Athletic Bilbao iliwaondoa Real Madrid kwenye michuano ya Copa del Rey baada ya kuifunga timu hiyo bao 1-0 siku ya Alhamisi usiku ndani ya uwanja wa San Mamés.

Bao la Berenguer dakika za majeruhi liliua matuamaini ya Real Madrid kushinda taji hilo ikiwa ni hatua ya robo fainali Athletic Bilbao ambao walikubali kupoteza katika fainali ya Spanish Super Cup kwa Los Blancos pia iliwatoa Barcelona katika hatua ya 16 bora ya michuano hiyo.
Real Madrid walipambana kutengeneza nafasi bila uwepo wa Kareem Benzema amabye anasumbuliwa na majeraha. Utatu wa Wabrazil Vinícius Júnior, Rodrygo na Casemiro walirejea kutoka kwenye majukumu na timu ya taifa lakini hawakuonyesha makali yao, Vinícius alitolewa mapema mwa kipindi cha pili kabla ya Casemiro kutoa boko ambalo lilileta madhara na kumpa nafasi Berenguer kufunga bao pekee la mchezo huo.
Real Betis pia walifuzu hatua inayofuata baada ya kuifunga bao 4-0 timu ya Real Sociedad siku hiyo hiyo ya Alhamisi.
Dakika tano pekee zinakutosha kuwa mmoja wa washindi wa mkwanja mrefu ndani ya kasino pendwa ya meridianbettz katika sloti maridhawa ya KENO, moja ya michezo inayoipa thamani dau lako.


