Rais wa shirikisho la mpira wa miguu Ulaya Aleksander Ceferin amewataka FIFA kuachana na mpango wa kucheza kombe la dunia kila baada ya miaka miwili huku akisema haufiki popote.
Mpango wa kuchezwa kombe la dunia kila baada ya miaka miwili ilikuwa ni wa raisi wa FIFA Gianni Infantino ambaye anajaribu kutafuta mashirikisho ya mpira wa miguu kumuunga mkono kwa kuwashawishi kuwa ikiwa mpango huo utafanikiwa basi shirikisho hilo litatengeneza kiasi cha 4.4 billion.

Raisi wa UEFA Aleksander Ceferin alipohokiwa na Financial Times kwenye mkutano wa Football Business Summit, alisema, FIFA wametambua mpango wao hautazaa matunda, nafurahi kuwa FIFA wametambua hilo pia,
Kombe la Dunia kila baada ya miaka miwili halitafika popote, milikuwa namazungumzo na rais wa FIFA, kuhusu hili jana, hatuwezi kuwasemea mpira wa bara jingine kuwa hauwezi kuendelezwa, lakini lazima viambatane, na wasiumize mashirikisho ya ulaya na Marekani ya kusini.
Tulizungumza lakini kwa sasa ninavyoongea, mpango wa kombe la dunia kila baada ya miaka miwili hakuna wazo hilo tena mezani, nina uhakika tutakuja na utatuzi na FIFA.
Haijawahi kuwa rahisi hivi kwenye safari yako ya kuvuna mkwanja, kasino maridhawa ya meridianbettz inakuletea mchezo wa Emoticoins unaokupa nafasi ya kufanya safari yako kuwa rahisi zaidi. Wakati ni wako nafasi ni yako na Emoticoins.


