Novak Djokovic Kushiriki French Open na Monte-Carlo Masters

Novak Djokovic anatumaini kushiriki kwenye mashindano ya French Open baada ya serikali ya Ufaransa kuondoa vikwazo vya chanjo ya Uviko-19 baada ya mwezi huu kupitisha sheria ya kutoruhusu mtu yeyeto kuingia pasipo kuchanja.

Mwezi January waziri wa michezo wa Ufaransa alitangaza kwamba wanamichezo wote wanahitaji kuchanjwa ili kuweza kushiriki michuano yeyote  ambayo itafanyika kwenye ardhi ya Ufaransa, hii iliondoa uwezekano wa Novak Djokovic kutetea taji lake la Roland Garros.

Novak Djokovic ni mchezaji pekee wa tennis kwenye wachezaji bora 100 ambaye hajachanja na alishindwa kutetea taji lake la Australian Open mapema mwaka huu, baada ya kusubili kwa muda mrefu kibali chake baada ya kuzuiwa hotelini kwa siku 11 jijini Melbourne.

Habari hii ni njema kwa Djokovic, ambaye pia ataweza kushiriki mashindano ya Monte-Carlo Masters mwanzoni mwa mwezi April, ambapo itakuwa mashindano yake makubwa ya pili mwaka huu.


KASINO YA MTANDAONI: EMOTICOINS SABABU YA KUVUNA ZAIDI.

Haijawahi kuwa rahisi hivi kwenye safari yako ya kuvuna mkwanja, kasino maridhawa ya meridianbettz inakuletea mchezo wa Emoticoins unaokupa nafasi ya kufanya safari yako kuwa rahisi zaidi. Wakati ni wako nafasi ni yako na Emoticoins.

senegal, Senegal Mabingwa AFCON 2021., Meridianbet

CHEZA HAPA.

Acha ujumbe