Rais wa Al Ahly Aomba Radhi Baada ya Kutolewa CAFCL

Klabu ya Al Ahly imetoa tamko rasmi kufuatia kuondolewa katika michuano ya CAF Champions League baada ya kufungwa jumla ya mabao 3-2 na ES Tunis, hatua iliyozua taharuki kwa mashabiki na wadau wa soka Nchini Misri na Afrika.

Rais wa Al Ahly Aomba Radhi Baada ya Kutolewa CAFCLKupitia kwa Rais wa klabu hiyo, Mahmoud El Khatib, uongozi umefanya kikao cha dharura na kukiri kuwepo kwa mapungufu ya kiufundi na kiutawala yaliyochangia matokeo hayo yasiyoridhisha katika mashindano hayo makubwa barani Afrika.

Bila kusahau meridianbet ndio wakali wa ODDS KUBWA, Machaguo zaidi ya 1000 na kila kitu ukitakacho. Bashiri kijanja hapa  

Katika hatua ya kurekebisha hali hiyo, klabu imesisitiza kuwa tayari imefikia maamuzi magumu yatakayohusisha mabadiliko mbalimbali, ambapo baadhi yatatangazwa hivi karibuni huku mengine yakisubiri kumalizika kwa msimu ili kulinda maslahi ya timu.

Rais wa Al Ahly Aomba Radhi Baada ya Kutolewa CAFCLAidha, uongozi umeeleza kuwa umeanza mchakato wa kufanya mageuzi makubwa ndani ya sekta ya soka ya klabu hiyo, yakilenga kurejesha ubora, utambulisho na hadhi ya Al Ahly kama moja ya klabu bora barani Afrika.

Ikumbukwe Al Ahly anashindwa kuingia fainali ya ligi ya mabingwa kwa mara ya pili mfululizo ambapo msimu jana bingwa alikuwa Pyramidi ya Nchini nmsri na mimu huu tayari ameshatolewa kwenye hatua ya robo fainali ya michuano hiyo.

Rais wa Al Ahly Aomba Radhi Baada ya Kutolewa CAFCLKatika hitimisho la tamko hilo, uongozi umeomba radhi mashabiki kwa huzuni na hasira waliyonayo kufuatia matokeo hayo, huku ukiahidi kuchukua hatua za haraka ili kurejesha mafanikio na imani ya wapenzi wa klabu hiyo

Acha ujumbe

Meridianbet
Privacy Overview

This website uses cookies so that we can provide you with the best user experience possible. Cookie information is stored in your browser and performs functions such as recognising you when you return to our website and helping our team to understand which sections of the website you find most interesting and useful.