Klabu ya PSG waliingia kwenye mgogoro baada ya kuyaaga mashindano ya Ligi ya Mabingwa ikiwa hatua ya 16 bora wiki iliyopita. Jambo moja ambalo ni la uhakika ni kwamba Nasser Al-Khelaifi atasalia kuiongoza klabu hiyo vilevile atasalia kusimamia miradi mbalimbali ya michezo ambayo imekuwa chini ya utendaji wake hadi sasa.
Al-Khelaifi sasa atasimamia mabadiliko katika muundo wa michezo wa PSG ili kutimiza lengo lao la kutwaa taji lao la kwanza la Ligi ya Mabingwa, na klabu hivi karibuni itafafanua mtindo wao mpya wa michezo na mustakabali wa Leonardo na Mauricio Pochettino.
Mkurugenzi huyo wa michezo alirejea klabuni hapo kuchukua nafasi ya Antero Enrique, lakini maamuzi yake ya hivi karibuni yametiliwa shaka sana.Kuhusu Pochettino, hakuna uwezekano kwamba atabaki kuwa kocha. Amebakiza mwaka mmoja kwenye mkataba wake, ingawa uamuzi kuhusu mustakabali wake umewekwa wazi.
Mbali na kuwa rais wa klabu ya PSG, Al-Khelaifi ni mwenyekiti wa beIN Media Group, mwenyekiti wa Qatar Sports Investments, rais wa Shirikisho la Tenisi la Qatar na makamu wa rais wa Shirikisho la Tenisi la Asia Magharibi mwa Asia.
Kuhusiana na hatma ya Mbappe, klabu hiyo inasubiri uamuzi wake kuhusu mustakabali wake katika klabu hiyo. Klabu inamsubiri aeleze nia yake kwa sababu, kama ataamua kutoongeza mkataba wake, watatafuta chaguzi mbadala katika dirisha la usajili la majira ya joto.
Maana ya ushindi mkubwa ipo hapa katika mchezo wa SHAOLIN FORTUNES 100 ndani ya kasino maridhawa za meridianbettz. Kwa dau dogo unashinda zaidi, unaweza kucheza mara nyingi uwezavyo huku ukifurahia ladha ya ushindi.


