Fowadi wa Barcelona Ansu Fati amerejea mazoezini na kikosi cha kwanza cha klabu kufuatia kuwa nje kwa muda mrefu kutokana na jeraha.

Mchezaji huyo wa miaka 18 alikosa nusu ya pili ya msimu wa LaLiga baada ya kuumia goti la upandewa kushoto mwezi Novemba 2020.
Fati alipata jeraha wakati wa ushindi wa 5-2 wa Barcelona dhidi ya Real Betis huko Camp Nou, na baadaye akafanyiwa operesheni tatu.
Lakini, mchezaji huyo wa kimataifa wa Uhispania anakaribia kurudi uwanjani baada ya kupigwa picha tena kwenye uwanja wa mazoezi kwenye uwanja wa mazoezi wa Barcelona Ciutat Esportiva Joan Gamper siku ya Jumanne.
Ingawa hatapatikana kwenye mchezo wa LaLiga wa wikendi hii dhidi ya Getafe, Fati anaweza kuwa kwenye safari ya Barcelona kwenda Sevilla mwezi Septemba 11.
Fowadi huyo alikua mfungaji mdogo zaidi katika historia ya Barca wakati alipofunga dhidi ya Osasuna mwezi Agosti 2019 akiwa na miaka 16 na siku 304.

Fati ameongeza mabao mengine 12 katika mechi 42 kwenye mashindano yote ya Blaugrana, ambaye alijiunga na umri wa miaka 10.
Kijana huyo aliyezaliwa Guinea-Bissau amecheza mara nne na timu ya Uhispania, na alifunga bao lake la kwanza la kimataifa dhidi ya Ukraine mwezi Septemba 2020.
Unawezaje kuikosa hii! Ndani ya kasino za meridianbet kuna mchezo unaoweza kukupa mkwanja mrefu leo hii, Wild Hot 40 ni njia nyingine ya kukufanya milionea, Chagua namba yako na uvune mkwanja.



[email protected]
Safi san