Nyota wa Rennes Eduard Camavinga amekiri kwamba “ni vizuri pale vilabu vikubwa vikivutiwa na wewe” ikiwa anahusishwa na mabingwa watetezi wa LaLiga Real Madrid.
Camavinga amekuwa akisita kuondoka katika klabu ya Lige 1 Rennes kwenda Real Madrid, ambao wamekuwa wakitamani kuinasa saini ya Camavinga.
Mbingwa watetezi wa Ligue 1 Paris Saint-Germain, mabingwa watetezi wa Serie A Juventus na Manchester Uited wote pia walikuwa wakivutiwa na kumnasa kiungo huyo wa 18.
“Ndiyo ni vizuri sana kama unatakiwa na vilabu vikubwa,” Camavinga aliiambia Canal ikiwa uvumi umezidi kuwa mkubwa kuhusus hatima yake. “Lakini mimi nakituliza kichwa.
“Mimi bado ni Rennes, tutasubiri mpaka mwisho wa msimu.
“Tutakutana mezani na tutapima hasra na faida kisha tutaamua.
Camavinga alicheza mchezo wa kwanza kwa timu ya vijana ya Rennes mwaka 2019 na haraka sana aliweza kuonesha kipaji chake na kikaonekana.
Mfaransa huyo amefunga goli moja na kutoa asisti 1 katika mechi 17 za ligi msimu huu na timu yake ipo katika nafasi ya 5 alama saba nyuma ya viongozi wa Ligue 1, Lyon baada ya kwenda nao sare ya 2-2 siku ya Jumamosi.
MERIDIANBET INAKUPA NAFASI YA KUWA MILIONEA KWA KILA BAADA YA DAKIKA 5
Mchezo wa Keno unakupatia fursa ya kuibuka kidedea kupitia droo zinazochezwa kila baada ya dakika 5 tu!! Tunaposema Meridianbet ni nyumba ya mabingwa, tunamaanisha!!
warda
Kizuri kinajiuza
Adelta
Anakubalika sana hongera yake
Rahmal
Yuko vizuli wanamkubali sana
Sania
Kiwango chake kimeongezeka
Magdalena
Ukiona mpaka virabu vikubwa vinakuhitaji ujue kiwango chako kimekua
Angelina
Kazi yake inaonekana
Sarah
Yuko makini sana
Dorophina
Madrid ni klabu nzuri kwake camavinga
Gabriel
Dogo yuko vzur sana
aisha
Yuko vizuri
Hopemwaikuka
True say
Ernest Kimeru
Muda wa Camavinga sasa
Lydia Emmanuel Magoti
Dogo anajua
Saupha mohamed
Jamaa yupo vizuri