Mwamuzi wa EPL Mike Dean anajipanga kustaafu mwisho wa msimu 2021/22 baada ya kuhudumu katika nafasi hiyo toka mwaka 2000.
Dean, mwenye umri wa miaka 53, ataingia katika jukumu la kuhudumu kama Mwamuzi Msaidizi wa Video (VAR) kabla ya kampeni ya 2022/23. Tayari amechezesha mechi 553 kwa ujumla na akitoa kadi nyekundu 114 nyingi zaidi kuliko mwamuzi yoyote, Dean pia amesimamia baadhi ya michezo mikubwa ya ligi hiyo.
Kwa mujibu wa taarifa mabli mbali Dean alipanga kustaafu mwaka uliyopita lakini baadaye alibadili mawazo yake pia Dean alifikisha kadi nyekundu namba 100 baada ya kumuonyesha Ashley Young wakati Man United walipocheza dhidi ya Wolves miaka mitatu iliyopita.
Una nafasi ya kupata bonasi ya shilingi 3500 kwa ajili ya kuanza safari yako ya kasino ya mtandaoni ya Meridianbet.