Mshambuliaji wa Liverpool Mohamed Salah hajataka kuongea chochote kuhusiana na hatima yake huko Anfield wakati huu ambapo mazungumzo ya kusaini mkataba mpya yanaendelea.
Mchezaji huyo wa kimataifa wa Misri amesema kwa sasa anaangazia kufikia malengo ya timu baada ya kuulizwa kama ataongeza mkataba na majogoo wa Anfield.
“Siwezi kusema ndiyo, siwezi kusema hapana lakini niliwahi kusema mara nyingi kuhusu kile ninakitaka,” Salah aliiambia Sky Sport.
“Kwa mara nyingine tena siwezi kwenda kiunda sana kuhsu mkataba sababu ni hali ya ndani zaidi.
Mkataba wa Salah unatarajiwa kuacha kufanya kazi mwaka 2023 na Liverpool wanaweza kumpoteza bila malipo katika dirisha la usajili la kiangazi kama asipo saini kandarasi mpya.
Maana halisi ya ushindi mkubwa unaipata katika kasino ya mtandaoni ya Aviator kutoka meridianbettz. Andaa kapu la ushindi wa mkwanja na beti kibao za BUREEE.