Michuano ya Europa League msimu huu inaanza kutimua vumbi na siku ya Alhamisi usiku timu kibao zitaonyeshana uwezo ikiwa ni hatua ya makundi, hapa acha tuangalie mchezo kati ya Leicester City dhidi ya Napoli utakaopigwa katika dimba la King Power.

Taarifa za timu:
Napoli wanatarajia kuwa bila nahodha wao Loreno Insigne ambaye alilazimika kutoka kwenye mechi dhidi ya Juventus wikendi ilyopita baada ya kupata jeraha la mguu.
Golikipa wa Napoli Alex Meret aliondolewa katika kikosi cha Italia wakati wa mapumziko wa michezo ya kimataifa baada ya kuumia mgongo kwa hivyo David Ospina atachukua jukumu langoni.
Luciano Spalletti pia Stanislav Lobotka wote watakuwa nje sababu ya jeraha la misuli, vilevile Diego Demme yupo nje kwa hiyo Andre-Frank Anguissa ambaye alifanikiwa sana kwenye mchezo uliyopita ataungana na Fabian Ruiz pamoja na Eljif Elmas.
Mfungaji wa rekodi Dries Mertens na beki Farouzi Ghoulam wote pia lakini Piotr Zielnski anapatikana sasa.

Kwa upande wa Leicester mejeruhi siyo wengi kama ilivyo kwa Napoli Ricardo Pereira ndiye mchezaji ambaye yupo sawa kutumika kama mbadala.
Beki wa kati wa The Fox Jannik Vestergaard bado anaendelea kupona kuwa sawa kabisa wakati Filip Benkovic amesajiliwa katika kikosi cha Europa League kitakacho menyana na Napoli.
Kunauwezekano wa James Maddison kuachwa katika mchezo wa leo baada ya kuchez mechi 15 bila kupata bao lolote wala kutoa asisti kwa hiyo Patson Daka au Kelechi Iheanacho ambao wamekuwa na viwango vya kuvutia wanaweza kuanza katika safu ya ushambuliaji.
Kikosi cha Leicester City Kinachoweza kuanza: Schmeichel; Castagne, Vestergaard, Soyuncu, Bertrand; Albrighton, Tielemans, Ndidi, Barnes; Daka, Vardy
Kikosi cha Napoli kinachoweza kuanza: Ospina; Di Lorenzo, Manolas, Koulibaly, Rui; Anguissa, Elmas, Ruiz; Politano, Osimhen, Lozano
Unaanzaje siku yako na kuimaliza bila kupitia katika kasino bomba za meridianbettz, mchezo mashuhuri wa Disco Funk unaweza kukufanya uwe mshindi leo hii.!


