Werner: Nahitaji Kufunga Goli la Kawaida Kwanza.

Timo Werner mshambuliaji wa Chelsea amekiri kwamba anaukame wa kufunga mabao licha ya kuchangia magoli yote katika ushindi wa wa Chelsea wa 2-1 dhidi ya Sheffield United.
Werner: Nahitaji Kufunga Goli la Kawaida Kwanza.
Timo Werner alipochezewa madhambi na mlinda mlango wa Sheffield United

Thomas Tuchel amendeleza wimbi la ushindi kwa Chelsea tangu achukue mikoba ya kuinoa timu hiyo mabao yaliyofungwa na Mason Mount na Jorginho na kufanya kukamilisha ushindi wa tatu mfululizo kwa bosi huyo mpya na kuisogeza Chelsea mapaka nafasi ya tano,

Lakini, licha ya The blues kufurahia ushindi huo Timo Werner alidaia kwamba alikuwa katika wakati mgumu na amekuwa akipambana kuzifumania nyavu kwa muda mrefu.

Alipoteza maoni kwamba alipaswa kupiga penati iliyofungwa na Joginho baada ya kuchezewa madhambi na golikipa wa Sheffield.

“Labda kwa siku zijazo naweza kupiga lakini kwa sasa, nahitaji kufunga magoli ya kawaida kwanza kabla ya kuanza kupiga penati,” alisema Timo Werner.

“Ilikuwa ni penati ya wazi na nilishangazwa kwanini haikuamuliwa moja kwa moja mpaka VAR ilipomsaidia refa.

Wakati huohuo, Werner alimsifia sana mataifa mwenzake Tuchel, ambaye amepata ushindi mara tatu mfululizo na kutoa sare katika mchezo wake wa kwanza akiwa kama kocha mkuu wa Chelsea.

“Kila kocha anatofauti, anatupa mawazo mengi na kwa sasa nacheza upande wa kushoto na naweza kucheza nyuma ya straika au kama namba kumi.


TENGENEZA MKWANJA UKIWA NA MERIDIANBET 

Unaweza kuvuna mkwanja mrefu kadiri uwezavyo kupitia mchezo wa Gold n Rocks kwenye  kasino ya mtandaoni ya Meridianbet. Ni rahisi! Vigezo na masharti, kuzingatiwa.

SOMA ZAIDI

14 Komentara

    Ndo ajitahidi sasa ila sio mbaya kwa kutoa asist

    Jibu

    Akazane Sana maana Chelsea awachelewi kumtema

    Jibu

    Timo inabidi haongeze juhudi

    Jibu

    Timo yupo vinzur na anaweza

    Jibu

    Nice update

    Jibu

    Werner anaongea sana hana vitendo kwa style yake labda wamuachie jukumu la kupiga penati

    Jibu

    Asante kwa taalifa

    Jibu

    Asante kwa taalifa

    Jibu

    Timo onyesha makali

    Jibu

    sawa

    Jibu

    Akaze najudi ziongezeke

    Jibu

    Ataweza akijitahidi na akiwa na nia .

    Jibu

    Anavosema Timo ni kweli inabidi afunge magoli kwani ni mda sasa toka afunge goli na yy ni mchezaji wa kimataifa

    Jibu

    Funga tu

    Jibu

Acha ujumbe

Meridianbet
Privacy Overview

This website uses cookies so that we can provide you with the best user experience possible. Cookie information is stored in your browser and performs functions such as recognising you when you return to our website and helping our team to understand which sections of the website you find most interesting and useful.