Zinedine Zidane hana mpango wa kumpumzisha mshambuliaji wa Real Madrid Karim Benzema kwani alisema atamchezesha Eden Hazard kidogo kidogo ili arejee kwenye mchezo kamili.
Benzema alishindwa kupiga shuti hata moja langoni katika ushindi wa 2-0 wa Madrid dhidi ya Celta Vigo kwenye LaLiga siku ya Jumamosi.
Mchezaji huyo wa miaka 33 ameanza katika mechi 15 kati ya 17 za LaLiga msimu huu ni kipa Thibaut Courtois pekee na Raphael Varane wamecheza dakika nyingi zaidi yake.
Alipoulizwa katika mkutano wa waandishi wa habari baada ya mechi ikiwa Benzema, ambaye amefunga mabao nane katika LaLiga, atahitaji kupumzika, kufuatia kiwango kidogo alichoonesha, Zidane hakukubali.
“Sidhani kama amechoka,” Zidane alisema.
“Nadhani alifanya vizuri na nikamchukua ili mchezaji mwingine acheze. Tuko katika uelekeo mzuri. Tunafanya vitu sahihi na lazima tuendelee hivi.”
Hazard alitokea benchi katika mchezo huo katika kipindi cha pili cha mchezo na ulikuwa mchezo wake mwingine baada ya kutoka kuuguza majeraha
“Tutakwenda kidogo kidogo,” aliongeza Zidane. “Kidogo kidogo, lazima urejeshe hisia.
“Polepole na sio kulazimisha chochote. Lazima arudi kwenye ubora wake na aichukue polepole. Ni hayo.”
VUNA SHEA YAKO YA 230,000,000TSH NA UFURAHIE MSIMU HUU WA SIKUKUU!!!
Kupitia Kasino ya Mtandaoni ya Meridianbet, jiwekee nafasi ya kupata shea yako ya 230,000,000Tsh kupitia mchezo wa Secret Santa. Hakika hutojutia kufurahia msimu huu wa sikukuu ukiwa katika nyumba ya mabingwa ya Meridiabet. Unasubiri nini?
Saupha mohamed
Maamuzi mazuri
Devotha
Benzema yupo vizuri
Hopemwaikuka
Muache apge kaz
Lydia Emmanuel Magoti
Safiii benzema yupo vizuri
Angelina
Nice update
Dorophina
Benzema yupo vizuri lazima apige kazi mwanzo mwisho
Magdalena
Benzema noma
Shakila mrope
Wamuache apige kaz
Adelta
Benzema Yuko makini
warda
Zidane huwa anamkubali sana benzema
Rahmal
Beneza Yuko vizuli
Ernest Kimeru
Ngoja tuone
Sania
Benzema bado yupo fiti
Issa
Benzema hafai