Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi wa Simba SC, Mo Dewji leo ameomba watu kumuunga mkono kumshawishi Raisi John Magufuli kuwa Uwanja wa Taifa kuitwa Benjamin William Mkapa kama sehemu ya kumbukumbu ya mchango wake katika ujenzi wa uwanja huo. ”Leo nimeamua kuanzisha petition (maombi) kwa Rais wetu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt John Pombe Magufuli kubadili jina la Uwanja wa Taifa kuwa: Uwanja wa Benjamin William Mkapa.
Ujenzi wa Uwanja wa Taifa wa jijini Dar es Salaam ulianzishwa na Rais wa Awamu ya Tatu, Benjamin William Mkapa. Uwanja huo wenye uwezo wa kubeba mashabiki 60,000 ni miongoni mwa viwanja bora katika bara la Afrika kwa sasa. Uwanja huo kwa namna mmoja au nyingine umesaidia kuendeleza mpira wa miguu na michezo mingine nchini Tanzania. Uzuri na ukubwa wa soka letu umedhihirishwa kwa sababu ya uwanja wetu huo ambao unashika nafasi ya 11 kwa ukubwa Afrika.
Uwanja huo wa kisasa umeongeza uzalendo mkubwa kwa kuwezesha maelfu ya mashabiki kuwa sehemu ya michezo yote mikubwa, pia umeongezea mapato kwa klabu zote na kutuletea heshima kubwa nchini na mifano ipo dhahiri. Kutokana na uzuri wa uwanja huo, klabu zote za nje ambao huja kucheza katika uwanja huo zimekuwa zikitoa sifa mbalimbali. Timu za mataifa makubwa kama Brazil zimecheza kwenye uwanja huo na kumwaga sifa mbalimbali.
Nje ya michezo, mashindano ya usomaji wa Quran yaliona mkusanyiko mkubwa zaidi kwenye mashindano makubwa ya kusoma Quran barani Afrika, hii nayo ilikuwa ni rekodi nzuri kwetu Watanzania. Nje ya michezo, mashindano ya usomaji wa Quran yaliona mkusanyiko mkubwa zaidi kwenye mashindano makubwa ya kusoma Quran barani Afrika, hii nayo ilikuwa ni rekodi nzuri kwetu Watanzania.
Tumeshuhudia matamasha mbalimbali makubwa kama matamasha ya Pasaka na Krsimasi yakifanyika hapo na lengo la yote hayo ni kuleta umoja na mshikamano miongoni mwa Watanzania. Itakuwa ni heshima kubwa kama uwanja wetu pendwa utaitwa jina la Uwanja wa Benjamin William Mkapa. Tunamuomba Rais John Pombe Magufuli aridhie kubadili jina la uwanja huo kwa heshima ya Hayati Mkapa ili tuendelee kumkumbuka kwa mchango wake mkubwa na hasa kwa vizazi vijavyo.
Tunawaomba Watanzania wote bila kujali ushabiki wa klabu muunge mkono kwa kuweka sahihi ili tumuombe Mhe Rais kubadilisha jina la uwanja huo uitwe Benjamin William Mkapa Stadium au Uwanja wa Benjamin William Mkapa.”
Nini kinachokupa raha kama michezo ya kasino ya mtandaoni? Hasa unapojua kuwa kuna ushindi, jackpot na mizunguko kibao ya bure.
Ungana na bwana Meridian kupata ushindi na burudani.
mwajumah
Ni wazo zuri sana #Meridianbettz
Theckla
Mawazo yake nimeyaelewa
Magdalena
Kwa alilolisema dewji ni la kweli ingependeza jina la mkapa kuwepo Ili kumuenzi
Salma ngende
Sio mabaya mawazo yake
felister
wazo zuri hii itasaidia vizazi vijavyo kwaajili ya kumbukumbu
devotha
wazo lake ni zuri
Neema juma
Inabidii hilo wazo litendewe kazi kwa kweli
jullie
Tajiri kashasema
Adelta
Wazo lake Ni sahihi
Lydia Emmanuel Magoti
Mawazo yake Mo nimeyakubali yapo sahii akika naili wanaweza wakalipitisha kwangazi zajuu
aisha
Ni sawa wazo lako mo ili tuendelee kumuenzi
Ernest
Ni wazo zuri na lenye mashiko katika Taifa letu, Binafsi namuunga mkono yani kwa Mzee Mkapa itapendeza sana.
Gabriel
Habar njema
Mwanahamisi
Wazo lake ni sahihi
Ester jackson
Mawazo mazuri ila uwamuzi tuwaachie serikali
Zuhura omary kindamba
Hajakosea kuomba ivo ila amecherewa sana tushazoea kuita uwanja wa taifa
Issa
Itakua kumbukumbu nzuri
Tatu
Habari njema
Fatuma kasomo
Wazo zuri
Furahav
Sawa tu,likiwekwa jina la mkapa.
lombo
sio mbaya
Hope mwaikuka
Mawazo yake tu sio lazma yatimie
Saupha mohamed
Wazo zuriiii
Genia Sikaluzwe
Siyo mbaya
Sadick
Lilikuwa wazo la Mkapa Uwanja wa kisasa ujengwe jambo ambalo tulidhani haliwezekani kwa miaka mingi. Ni jambo la heshima uwanja kupewa jina la hayati Mkapa kumuenzi#meridianbettz
Rose kapinga
Ni vizur kufanya ivyo inaleta heshimaa!!
Povel
Kwl wawez kumuwenz mzee wetu na kumpa heshimah yake
Amiri Kayera
Itakua kumbukumb nzur zaid
Shafii
Sio jambo baya .
JULIANA
Kwani kabla ya apo sindio unavyoitwa uwanja wa mkapa na sio wa mchina
MnonganeJR
Tajiri mo tupo pamoja na wewe kwa wazo lako#meridianbettz
sabrina
Ni jambo zuri
Tahiya
Mawazo yake yafanyiwe kazi
Rehema
Yuko sahihi kwa mawazo yake
caroline
kila na mtu na mawazo yake
warda
Sio mbaya lakini#Meridianbettz
Zeiyana
Litakua jambo bora sana kwani kumbu kumbu zake zitakua kwa vizazi vijazo na mchango wake katika nyanza za michezo.
Omary lukumbi
Sio mbaya
Dorophina
Moo yupo sahihi itakuwa km kumbu kumbu za kumuenzi mh mkapa
Janeflora malisa
Mo yupo sahih
David Pere
Aliomba hivyo na umekuwa hivyo so toka Sasa ni mkapa stadium
Theonestina
Mawazo take yamekubarika
Shan
Habar njema