Jack Wilshere Atundika Daluga Akiwa na Miaka 30

Kiungo wa zamani wa Arsenal na timu ya taifa ya Uingereza Jack Wilshere ametangaza kustaafu kucheza soka la kitaalamu na kugeukia katika ukufunzi.

Jack Wilshere Atundika Daluga Akiwa na Miaka 30

Wilshere ambaye ana umri wa miaka 30 amestaafu akiwa bado na umri mdogo na wiki ijayo atatangazwa kuwa kocha mpya wa timu ya vijana chini ya umri wa miaka 18 ya Arsenal.

Mchezaji huyo wa zamanik wa Bolton, Bournermouth na West Ham United aliichezea mechi 13 timu ya Aarhus inayoshiriki ligi ya Denmark msimu uliyopita.

Wilshere aliandika kwenye akunti yake ya Twitter: “Leo natangaza kustaafu kucheza mpira wa miguu, hakika imekuwa safari isiyoaminika ambayo imejazwa na nyakayytio nyingi.Kutoka kuwa mtoto mdogo niliyecheza mpira kwenye bustani mpaka kuja kuwa nahodha wa timu ya ngu pendwa ya Arsenal na kuichezea timu ya taifa langu kwenye michauno ya Kombe la Dunia. Hakika nimeishi ndoto yangu.


BASHIRI HAPA KWA ODDS KUBWA NA MACHAGUO MENGI ZAIDI

Acha ujumbe