Kyle Walker ana shaka kubwa kulikosa Kombe la Dunia baada ya kufanyiwa upasuaji wa paja wiki hii.
Nyota huyo wa Manchester City alikosa mechi yao ya Ligi ya Mabingwa Ulaya dhidi ya Copenhagen Jumatano usiku na baada ya mchezo huo Pep Guardiola alisema atakuwa nje kwa muda.

“Sijui [muda gani]. Siwezi kusema chochote kingine. Inabidi tuzungumze na madaktari. Natumai anaweza kurudi kama Kalvin [Phillips]. Najua jinsi Kombe la Dunia lilivyo muhimu kwa wachezaji lakini kusema kweli sijui kwa sasa.”
Walker alitweet Alhamisi asubuhi: “Kama mchezaji tunapaswa kufahamu majeraha ni sehemu ya mchezo tunaoupenda. Operesheni yangu siku ya Jumanne ilifanikiwa na sasa ninaweza kuelekeza nguvu kwenye kujiweka sawa na kurejea kwenye utimamu kamili. Nitakuwa nikiwasaidia wachezaji wenzangu kila siku kwa njia yoyote niwezayo.”

Habari hizi zitakuwa na wasiwasi mkubwa kwa kocha wa England Gareth Southgate kutokana na umuhimu wa Kyle kwenye mipango yake. lakini kwa habari za chini zinasema, bado kuna matumaini kuwa beki huyo wa kulia anaweza kuthibitisha utimamu wake kabla ya Kombe la Dunia.

