Kocha mkuu wa Juventus Andrea Pirlo amesema mabingwa hao wanaoshikiria ubingwa wa Serie A lazima wajifunze kushinda bila uwepo wa Christiano Ronaldo baada ya supastaa huyo kuukosa mchezo wa Jumamosi dhidi ya Benevento.
Ronaldo alipumzishwa wikendi hii na juve ilishindwa kufanya vizuri kwa kulazimishwa sare ya 1-1 Juve walipokuwa ugenini.
Goli la ufunguzi la Alvaro Morata dakika ya 21 ya mchezo lilisawazishwa dakika ya 45 na mchezaji wa Benevento Gaetano Letizia kabla ya mchezaji huyo hajatolewa.
Juventus wapo nyuma ya viongozi wa Serie A kwa tofauti ya alama tatu na pirlo hajafurahishwa na kiwango cha wachezaji wake na amewataka kuimarika hata bila uwepo wa Ronaldo – ambaye amefunga magoli nane katika michezo mitano ya Serie A msimu huu.
“Ronaldo nimchezaji muhimu sana, sio tu kwetu sisi,” Pirlo aliongea na maripota baada ya mechi.
“Alikuwa ana umuhimu hata katika klabu ya Real Madrid.
“Aina hii ya mchezaji ambaye anafikia malengo, lakini lazima tujifunze kufanya vizri hata bila uwepo wake.
Juve wameshinda mchezo mmoja pekee katika michezo tisa ya ugenini kwenye Serie A.
Wababe hao wa Italia ambao wameshinda mechi nne na kutoa sare tano, na wamefikia idadi ya michezo waliyotoa sare msimu uliyopita pia ameirudia rekodi ya mwaka 2001-02 kutoa sare tano katika mechi tisa.
“Siogopi, lakini lazima tufikirie kwamba michezo inaendelea na tayari tumepoteza alama nyingi.
Hadi 130,000,000 TSH Kutolewa kwa washiriki wa shindano la Playson Cashfall. Unaipata kwenye Kasino ya Mtandaoni ya Meridianbet Pekee. Jisajili sasa, kisha ingia mchezoni kabla ya Novemba 29.
Lydia Emmanuel Magoti
Nikweli yupo sahii
Nasra
Hii ni sawa kabisa
Sadick
Pirlo atajikuta yupo nje ya dimba endapo ataendelea na majaribio yake ya kikosi, hakuwa na sababu kumwacha nje Ronaldo
Issa
Timu haitakiw tegemea mtu mmoja
lombo
sahh
Adelta
Yupo sahii
Dorophina
Ni sawa kabisa juve inabidi wajifunze kucheza bila ronaldo wawe na imani kama wataweza
Sauda
Kweli kabisa
Magdalena
Kabisa maana Luna Sikh Rinaldo asiwepo
Mariam mtandama
Kweli
Fatuma kasomo
Gud
Rahma
Kweli
Hopemwaikuka
Kabsaa
Tatu
Kocha yupo sahihi
Tahiya
Kabisa yaani
warda
Kwa kweli