Kocha wa Yanga Princess atamba

Kocha Mkuu wa Yanga Princess, Sebastian Nkoma amesema kuwa angekuwa na timu hiyo kwa wiki tatu Simba wasingepata sare ya jana.

Jana ulipigwa mchezo wa ligi kuu ya wanawake kati ya Simba Queens dhidi ya Yanga na kumalizika kwa sare ya bao 1-1.

Kocha wa Yanga Princess atamba

Akizungumza baada ya kumalizika kwa mchezo huo, Nkoma alisema anawapongeza wachezaji wake kutokana na kiwango kizuri walichokionyesha kwenye mchezo huo.

Kocha wa Yanga Princess atamba

“Kwanza nawapongeza wachezaji wangu kwa mchezo mzuri na kufanikiwa kupata pointi moja kutokana na maelekezo niliyowapa.

“Hiyo Simba unayoiona nimeiandaa mimi sasa endapo ningepata muda zaidi wa kukiandaa kikosi changu hata kwa wiki tatu wasingepata hii sare.”

Acha ujumbe