Kocha Mkuu wa kikosi cha Ruvu Shooting, Charles Mkwasa amefunguka kuwa matokeo waliyopata jana yametokana na wachezaji kucheza chini ya kiwango.
Jana Ruvu Shooting walipoteza mchezo wa ligi uliopigwa Uwanja wa Uhuru dhidi ya Mbeya City kwa bao 1-0 lililofungwa na Hassan Nassoro.
Akizungumzia mchezo huo, Mkwasa alisema “Kwanza niseme tunamshukuru Mungu mchezo umemalizika salama, matokeo ya leo yametokana na wachezaji kucheza chini ya kiwango.
“Wachezaji karibu wote kwenye kikosi walicheza chini ya kiwango kitu ambacho kimeigharimu timu kukosa matokeo licha ya nafasi nyingi ambazo tumezitengeneza.
“hata bao ambalo tumeruhusu limetokana na umakini mdogo kwenye safu ya ulinzi lakini tunarudi kwenye Uwanja wa mazoezi kwa ajili ya kuangalia namna ya kurekebisha hilo.
“Hakuna kocha ambaye anapenda timu yake ifungwe lakini inatokea kutokana na makosa ambayo yanafanyika wakati wa mchezo.”