Polisi Kuipeleka Singida Karatu

Mchezo wa ligi kuu kati ya Polisi Tanzania dhidi ya Singida Big Stars sasa utapigwa kwenye Uwanja wa Black Rhino uliopo Karatu, Arusha.

Sababu ya mabadiliko ya uwanja ni baada ya kufungiwa kwa uwanja wa Sheikh Amri Abeid ambao ulikuwa ukitumiwa na Polisi Tanzania kama uwanja wao wa nyumbani.

Akizungumzia mabadiliko hayo, Ofisa Habari wa Polisi Tanzania, Hassan Juma amesema kuwa watautumia uwanja huo kwa mchezo dhidi ya Singida Big Stars.

“Kikosi kinaendelea na maandalizi ya mchezo ujao wa ligi dhidi ya Singida Big Stars, utakuwa mchezo mgumu ila tunahitaji pointi tatu ambazo ni muhimu kwetu.

“Baada ya uwanja wa Sheikh Amri Abeid kufungiwa kwa sasa tutautumia uwanja wa Black Rhino uliopo Karatu kwa ajili ya mchezo huo.

“Tayari marekebisho ya uwanja wetu wa nyumbani wa Ushirika yamekamilika tunachosubiri kwa sasa ni ruhusa kutoka bodi ya ligi hivyo tuna imani baada ya kumalizika kwa mchezo ujao mechi nyingine tutacheza Moshi.”

Acha ujumbe

Meridianbet
Privacy Overview

This website uses cookies so that we can provide you with the best user experience possible. Cookie information is stored in your browser and performs functions such as recognising you when you return to our website and helping our team to understand which sections of the website you find most interesting and useful.