Wan Bissaka Kutimkia West Ham

Beki wa klabu ya Manchester United Aaron Wan Bissaka anatarajiwa kutimka ndani ya klabu ya Manchester United na kujiunga na klabu ya West Ham United kutoka jijini London.

Klabu ya West Ham inaelezwa wapo mbioni kutuma ofa kwa Manchester United ambao nao wako tayari kumuachia beki huyo, Kwani ni moja ya wachezaji ambao wamepanga kuwaachia klabuni hapo lakini pale tu watakapopata kiwango sahihi cha pesa ambacho wanakitaka.Wan bissakaKlabu ya West Ham wanapaswa kutoa kiasi ambacho kitawashawishi Man United kumuachia beki huyo mwenye asili ya Congo, Wagonga nyundo wa London wanaelezwa wameandaa kiasi cha paundi milioni 15 kwajili ya kupata huduma ya beki Wan Bissaka kuelekea msimu ujao.

Klabu ya Manchester United mpaka sasa wameshakamilisha usajili wa wachezaji wawili ambao ni mshambuliaji Joshua Zirkzee na beki Leny Yoro, Huku usajili mwingine ambao wanataka kuufanya itategemeana kwa kiwango kikubwa na wachezaji ambao watawauza hivo ni wazi United watahakikisha wanamuuza Wan Bissaka ili waendelee kufukuzia dili la mchezaji mwingine.

Acha ujumbe

Meridianbet
Privacy Overview

This website uses cookies so that we can provide you with the best user experience possible. Cookie information is stored in your browser and performs functions such as recognising you when you return to our website and helping our team to understand which sections of the website you find most interesting and useful.