Alaba Athibitisha Kuachana na Bayern Baada ya Miaka 13.


 

Beki kisiki wa Bayern Munich, David Alaba amethibitisha kuwa ataondoka katika klabu hiyo ya Bavaria mwishoni mwa msimu huu.

David Alaba amethibitisha kuwa ataondoka Bayern Munich mwishoni mwa msimu baada ya kuwepo klabuni hapo kwa takribani miaka 13.

Mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 28 ataondoka Allianz Arena kwa uhamisho wa bure mara tu mkataba wake na mabingwa wa Bundesliga utakapomalizika mnamo Juni.

 

Real Madrid, Chelsea na Liverpool zote zimehusishwa kumsajili beki huyo, lakini mchezaji huyo wa kimataifa wa Austria bado hajasema anapoelekea.

Akizungumza kwenye mkutano wa waandishi wa habari ambao haukupangwa, Alaba alisema: “Nimefanya uamuzi wa kuondoka Bayern mwishoni mwa msimu huu na kujaribu kitu kipya.

Ni wazi haukuwa uamuzi rahisi, nimekuwa hapa kwa miaka 13 na klabu hii imekuwa kila kitu kwangu, hivyo ninashukuru kwa mengi sana na ndio sababu nasema uamuzi huu kwangu umekuwa mgumu sana. Ninaweza kusema Bayern ni familia yangu.” aliongeza Alaba.


WEWE NI SHUJAA? MASHUJAA WANASHINDA HAPA!

Treasure Heroes inakupa nafasi ya kupambania ushindi wako mkubwa kwenye kasino ya mtandaoni ya Meridianbet! Usisubiri hii, jiunge sasa kufurahia ushindi!

Kasino ya Mtandaoni

INGIA MCHEZONI

12 Komentara

    Nice update

    Jibu

    Safi

    Jibu

    Safii

    Jibu

    Sio mbaya ni jambooo la kheri pia

    Jibu

    All ze best to him

    Jibu

    Safii

    Jibu

    Alaba haende tu liverpool

    Jibu

    Apambaneee

    Jibu

    Nice

    Jibu

    Ni sawa tu

    Jibu

    Alaba ameiga mfano wa Thiago Alcantara aliyeamua kuondoka Bayern Munich. Bayern Munich inatakiwa kusajiri msimu ujao.

    Jibu

    Angekuja Man U jamani

    Jibu

Acha ujumbe