Alex Telles Atimkia Sevilla

Mchezaji walimataifa wa Brazili anayekipiga kwenye klabu ya Manchester United Alex Telles leo amekamilisha uhamisho wke wa mkopo kutoka klabu hiyo kwenda Sevilla kwa mkopo wa muda mrefu.

Mchezaji huyo mwenye miaka 29, alijiunga na Manchester United akitokea FC Porto mwaka 2020 na amefanikiwa kuichezea klabu hiyo michezo 50 kwenye mashandano yote.

Alex Telles muda mwingi amekuwa akicheza beki namba tatu, baada ya mchezaji wa kimataifa wa Uingereza kuumia Luke Shaw. Kuwasiri kwa Tyrell Malacia kunamfanya akose namba kwenye klabu hiyo.

Sevilla wamekubali kugharamia mshahara wake wote na kwenye mkataba ambao amesaini Telles hakuna kipengere cha kumsajiri mchezaji huyo moja kwa moja kwenye klabu hiyo.

 

Acha ujumbe

Meridianbet
Privacy Overview

This website uses cookies so that we can provide you with the best user experience possible. Cookie information is stored in your browser and performs functions such as recognising you when you return to our website and helping our team to understand which sections of the website you find most interesting and useful.