Aliyekuwa nyota wa Man United, Alexis Sanchez alitaka kuondoka Manchester United mapema kabisa, baada ya mkataba wake na Manchester City kushindwa kufanya kazi.
Januari 2018, Manchester City walikuwa wanatarajia kumsajili Sanchez akitokea kwa washika mtutu Arsenal, lakini dili lilienda kuwa tofauti kabisa na akajikuta ametimba kwa wapinzani wao Man United kwa dili la mabadilishano na Henrikh Mkhitaryan.
Nyota huyu alipofika Man United alishindwa kuonesha ubora ule ule aliokuwa nao alikotoa, ambako alichukuliwa kama miuongoni mwa washambuliaji wa kali zaidi wa ligi ya Uingereza. Alikuwa analipwa £390,000 kwa wiki.
Katika mechi 45 alizocheza na United aliambulia magoli 5 tu! Tofauti na ambavyo wengi walitarajia, kisha akapelekwa Inter Milan kwa mkopo msimu wa 2019-20, kabla hawajakamilisha dili la kudumu katika dirisha hili la uhamisho.
Nyota huyu alikuwa akipata shida ya majeraha, lakini anabainisha kuwa hakujiona akifurahia mazingira ya Manchester United tangia awali kabisa.
Kupitia ukurasa wake wa Instagram, Alexis Sanchez aliamua kuweka bayana baadhi ya mambo ambayo anaamini mashabiki na wapenzi wa soka walikuwa hawayafahamu alipokuwepo United. Na pengine mambo hayo yalimfanya aonekane mbaya.
Chaguo la kwanza la Alexis Sanchez ilikuwa ni Manchester City
Sanchez alitamani zaidi kuwepo Manchester City. Licha ya kujikuta tayari alikuwa ameshatua United, ameyasema haya ya moyoni;
“Kabla ya kwenda kule [United] nilikuwa na makubaliano na Manchester City, lakini hii haikwenda sawa na nikapata nafasi ya kujiunga na Manchester United. Ilikuwa kitu kizuri ni klabu niliyoipenda nikiwa mtoto. Hatimaye nilisaini bila kuuliza nini kinatokea ndani ya klabu.”
“Kuna mambo ambayo hauwezi kuelewa mpaka uwepo pale, nilielewa mengi siku ya kwanza nilipokuwa mazoezini.” -Alexis Sanchez
Alexis Sanchez anasema kuwa aliwaambia familia yake na wakala kuwa hakuna uwezekano wa kurejea Arsenal? na ikachukuliwa kama utani. lakini hakufurahia kadri siku zilivyosonga. Alitaka aondoke.
SHINDA NA HI LO
Sasa hii ni rahisi zaidi kupata USHINDI! Unatabiri karata ipi ipo chini au juu, kisha unakusanya mkwanja wako.


Hope mwaikuka
Siku nyngne utulize akili zako ili uwe na aman ya moyo
Neema
Duu hii kaliii
Rose kapinga
Mambo ya soka hayo!!!
Sabrina
Duuuh hatarii
Agness
Asichukue maamuzi Kwanza atulie
Issa
Sanchez united hakuitendea haki
Sauda
Afikiri kabla ya kutenda
Fatina mfigi
Kam unaona hakuna masilai inasepa tyu!
Dorophina
Sanchez hakuna chochote alicho kitendea man u Ni bora haende tu kama anataka kuondoka hana mchango wowote kama klabu ilivyofikilia kwamba atakuwa na msaada
magdalena
sanchez nae aache tamaa atulie apo alipo panamfaa
Povel
Duh noma sana hiii
Ernest
Mara nyingi changamoto kama hizi wachezaji wengi wamekuwa wakikutana nazo hasa pale wapotoka kwenye timu moja kwenda nyingine ila kiukweli mbali na yote haya Sanchez hakuwa na msimu mzuri Old Trafford huenda ikawa imechangiwa na kukosa furaha
Adelta
Ni kweli Alexis Sanchez amekutana na changamoto bora aondoke tu@meridianbettz
Janeflora malisa
Changamoto kubwa
felister
wahenga walisema fikiria kabla hujatenda ona sasa yaliyomkuta sanchez
Nasra
Changamoto sanaa
Caroline
Alex kapata Sana majeraha msimu uliopita
Tatu
Sanchez nae alitaka kuondoka man u ndio maana akucheza vizuri
Mwanahamisi
Changamoto kubwa
Mwajumah
Duuh Mambo ya soka ayo yametaladadi#Meridianbettz
lombo
asante meridianbet kwa habar moto moto
Flomena
Nyota huyu alipofika Man United alishindwa kuonesha ubora ule ule aliokuwa nao alikotoa, ambako alichukuliwa kama miuongoni mwa washambuliaji wa kali zaidi wa ligi ya Uingereza. Alikuwa analipwa £390,000 kwa wiki.
aisha
Duuh majanga hayo endelea tuu hapo hapo
Saupha mohamed
Atulie tu man u
[email protected]
Du ndio changamoto izo
Lydia Emmanuel Magoti
Kipige tuu Man U panakufaa krabu kubwa iyo pambana Napo hapo hapo
Amiri Kayera
Kwa style ya United Sanchez pale haikua sehem sahii
David Pere
Sanchez alitamani zaidi kuwepo Manchester City. Licha ya kujikuta tayari alikuwa ameshatua United, ameyasema haya ya moyoni;
Sadick
Maneno hayo yanamaanisha alipoteza imani mara baada ya kujiunga Man U pengine ndio maana hakupata mafanikio#meridianbettz
Gabriel
Sanchez united hakuitendea haki
Khadija
Hatari#meridianbettz
warda
Acha asepe tu
Furahav
Mmh